Shusho: Kuwa karibu na Harmonize sio tatizo kwangu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Shusho na Harmonize

Mwimbaji mkongwe wa muziki wa Injili Tanzania, Christina Shusho amesema kuwa kwa miaka mingi amekuwa karibu na wasanii wakubwa kama Diamond Platnumz na Harmonize, hivyo haoni kama kuna tatizo kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakisema.


"Mimi sijali watu watasema nini kikubwa najua ninachofanya siyo dhambi, kwa nyakati tofauti nimekaa na Diamond Platnumz na nimekaa na Harmonize, hawa ni watu poa sana tofauti na watu wanavyowachukulia mitandaoni.


"Nimekaa na Harmonize sana hasa kipindi cha mgogoro wake na Kajala nilimshauri vitu vingi sana lakini hata siku moja hajawahi kumzungumzia vibaya Diamond, zaidi anamsifia na anamshukuru kwa kumfikisha alipo leo.


"Mimi kumuita Nabii Mkuu Geordavie "Mfalme" siyo shida, na wanaojaji lile tukio wana elimu ndogo ya dini, wana msongo wa mawazo hawajui wanachokizungumza wanaona wakinisema ndio mioyo yao inapona, Geordavie ni baba yangu wa kiroho tumetoka mbali sana, amenilea sana siwezi kuacha kuwa karibu nae.


"Nimezunguka dunia nzima nimebakisha mabara mawili tu ila sipendi kujionyesha kwa sababu mimi siyo mtu wa kujigamba, lakini nina watu karibia dunia nzima.


"Nimetoa Album yangu mpya inaitwa (Hararat) ina nyimbo 24 na inapatikana YouTube naomba mkasikilize nyimbo hizo," amesema Christina Shusho, Msanii wa muziki wa Injili Tanzania.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad