Tanzania Rapa pekee anaweza nishinda ni Professor Jay - Stevo Simple Boy

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Tanzania Rapa pekee anaweza nishinda ni Professor Jay - Stevo Simple Boy
 

Rapa wa Kenya Stevo Simple Boy amekumbatia mzozo wa vita vya maneno baina ya Sanaa ya Hip Hop ya Kenya na ile ya nchi jirani ya Tanzania.



Katika mahojiano na wanablogu wa habari za mitandaoni, Stevo alisema kwamba rap ya Tanzania haina mashiko hata kidogo kwani wao hurap kwa lugha ya Kiswahili ambayo haivuki kupita Mlima Kilimanjaro.


Stevo alisema kuwa nchini yeye na Khaligraph Jones ndio wafale pekee wa muziki huo wa rap akisema kuwa katika Sanaa ya rap ya Tanzania, haoni msanii yeyote ambaye anaweza kumkalisha kitako.


Stevo alisema mkongwe Professor Jay ndiye msanii peke anayeweza kumtingisha kidogo tu lakini wengine akawataja kama baridi ya msimu tu inayopita.


“Hamna msanii wa rap hata mmoja anayeweza nitoa kwenye ulingo. Labda tu mtu mmoja tu ndio anaweza nitoa. Mkongwe Professor Jay pekee yake. Hawa wengine ni bure tu. Rosa Ree bado ni mdogo sana na haniwezi,” Stevo Simple Boy alisema.


Stevo aliwahimiza wasanii marapa wa Kenya kujitosa kabisa kwenye ulingo wa kupambana kimaneno katika rap battle akisema kuwa hiyo ndio njia pekee ya kuiheshimisha Sanaa ya Kenya haswa kwenye kitengo cha rap.


Stevo alisema kuwa ana mpango wa kufunga safari kwenda Tanzania ili kuwaonesha kivumbi marapa wa huko ili kujizolea heshima.


“Watu walikuwa wanasema Stevo Simple Boy aingilie kati. Sasa natangaza pia mimi nimeingilia rasmi. Hata kama OG hajamaliza hiyo bifu, basi mimi nitaingilia niende mpaka pale Tanzania niwabwage hao marapa wote watukome. Mimi naingia kama amiri jeshi mkuu. Sisi tunaangalia ubabe wa Tanzania na Kenya, ni nchi gani ina marapa ambao wana uwezo mkubwa wa kuchana,” alisema.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad