AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kocha Mkuu wa Mabingwa wa Soka nchini Algeria Chabab Riadhi de Belouizdad ‘CR Belouizdad’, Marcos Paqueta raia wa Brazil amejikuta akiweka wazi mapema kuwa anatarajia mchezo mgumu dhidi ya Mabingwa wa Soka Tanzania Bara Young Africans kutokana na ratiba yao kubana.
CR Beluoizdad ambao ni wapinzani wa Young Africans katika ligi ya mabingwa Barani Afrika kutokana na kupangwa pamoja katika kundi D la michuano hiyo pamoja na timu za AI Ahly kutoka Misri na Madeama kutoka Ghana.
Akizungumza baada ya kupokea kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa USM Alger katika mchezo wa ligi kuu mwishoni mwa juma lililopita, kocha huyo alisema: “Ratiba haijakuwa rafiki kwetu ukitazama hapo mbeleni utaona kuwa tuna michezo mingi migumu mbele yetu lakini bado tumecheza mechi mfululizo.
CR Belouizdad kabla ya kukutana na Young Africans wanatarajiwa kukutana na michezo mingine miwili ya ligi kuu nchini Algeria dhidi ya Paradou FC Novemba 14 kisha Novemba 15 dhidi ya JS Kabylie.
Baada ya hapo CR Belouizdad watacheza mchezo wao dhidi ya Young Africans Novemba 24 wakiwa nyumbani kwao nchini Algeria.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK