Ndege zagongana Japan, watano wafariki dunia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Japan. Watu watano waliokuwa kwenye ndege ya walinzi wa Pwani ya Japan wamefariki dunia baada ya ndege yao kugongana na ndege ya abiria katika uwanja wa ndege wa Haneda jijini Tokyo.

Kwa mujibu wa tovuti ya BBC, Ndege hiyo ilikuwa ikipeleka msaada katika maeneo yaliyokumbwa na tetemeko kuu la ardhi la Januari 1, 2024.

Watu wote 379 waliokuwa kwenye ndege ya abiria inayomilikiwa na shirika la ndege la Japan Airways iliyowaka moto katika ajali hiyo, waliokolewa.

Picha za video zilionyesha abiria wakitoka katika mlango maalumu wa dharula wa ndege katika harakati za kujaribu kuokoa uhai wao.

Kufuatia tukio hilo, Waziri Mkuu wa Japan, Fumio Kishida amezungumza na waandishi wa habari na kuthibitisha wafanyakazi watano kati ya sita kwenye ndege ya walinzi wa pwani walifariki dunia wakati wakiendelea na shughuli ya kupeleka msaada kwa watu walioathirika na tetemeko la ardhi la jana Jumatatu.

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa kipimo cha richa 7.6 lilipiga Japan siku ya mwaka mpya saa 4:10 asubuhi saa za ndani wakati watu wengi walikuwa wakitembelea familia na kusherehekea na kusababisha vifo na uharibifu mkubwa wa majengo na miundombinu.

Imeandaliwa na Victor Tullo kwa msaada wa mashirika.


----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad