AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Timu ya Simba SC imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Mapinduzi baada y ushindi wa penalti 3-2 dhidi ya Singida Fountain Gate leo Uwanja wa New Amaan Complex, ZanzÃbar.
Singida Fountain Gate ilitangulia kwa bao la mshambuliaji Mkenya Elvis Rupia dakika ya 11, kabla ya kiungo Mkongo Fabrica Luamba Ngoma kuisawazishia Simba SC dakika ya 90 na ushei.
Na kwenye mikwaju ya penalti kipa wa Simba SC, Ali Salim aliyeokoa penalti za mabeki Gardiel Michael, Hamad Waziri na mshambuliaji Mnyarwanda Meddie Kagere kuipa Simba tiketi ya Fainali Kombe la Mapinduzi.
Waliofunga penalti za Simba ni viungo Luis Jose Miquissone, raia wa Msumbiji, Israel Patrick Mwenda na Moses Phiri, wakati ya Shomari Kapombe iliokolewa na ya Mrundi, Saido Ntibanzokiza ikagonga mwamba wa juu na kwenda nje.
Ni viungo, Mkenya Duke Abuya na mzawa, Deus Kaseke pekee waliofunga upande wa Singida Fountain Gate.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK