Diwani Afariki Ghafla....

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Musoma. Diwani wa Kisorya katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Amos Ndaro amefariki dunia.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Charles Manumbu amethibitisha kutokea kwa kifo hicho usiku wa kuamkia leo Machi 15, 2024.

Manumbu amesema kifo cha diwani huyo ni cha ghafla, kwani hadi jana hakuwa na tatizo lolote la kiafya.

"Nimeongea naye jana, kuna mambo alitaka ufafanuzi lakini pia alikuwa na vikao kwenye kata yake ambavyo alivifanya hadi mwisho. Ninachoweza kusema mwenzetu amelala na Mungu ndiye anapanga saa ya kumchukua mja wake" amesema.

Amesema mwili wa marehemu umepelekwa hospitalini kwa uchunguzi zaidi na kwamba baada ya uchunguzi watajua kwa undani chanzo cha kifo hicho na taratibu za mazishi.

"Nipo njiani naelekea huko, nadhani nikifika nitajua chanzo ni nini maana mwili tayari umepelekwa hospitalini kwa uchunguzi. Nimepokea taarifa za kifo saa 10.45 alfajiri na nimeambia amefariki nyumbani saa 9," amesema.

Diwani wa Kibara katika halmashauri hiyo, Mtamwega Mgahwa amesema taarifa za awali zinadai diwani huyo amefariki dunia kwa tatizo la shinikizo la damu.

"Ameugua ghafla usiku na kufariki dunia usiku huo huo, lakini jana kutwa nzima alikuwa mzima na aliendelea na shughuli zake kama kawaida,"amesema.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad