Simba Wampa "Thank You" Kocha Benchikha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

BREAKING: Simba wampa "Thank You" Kocha Benchikha
Simba wampa "Thank You" Kocha Benchikha

Simba wampa "Thank You" Kocha Benchikha

Klabu ya Simba imetangaza rasmi kuachana na Kocha wake Mualgeria Abdelhak Benchikha baada ya miezi mitano tu tangu ajiunge na Wekundu hao wa Msimbazi.


Simba inaachana na Benchika siku moja tu tangu Mualgeria huyo aiwezeshe kutwaa Kombe la Muungano kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Azam FC jana usiku Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzíbar.


Aliwasili mwishoni mwa mwezi Novemba akasaini mkataba wa miaka miwili Novemba 28 kabla ya kuiwezesha timu kufika Robó Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambako ilitolewa na mabingwa watetezi, Al Ahly.


Lakini Simba ikatolewa katika Hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano ya ambayo sasa inajulikana kama CRDB Bank Federation Cup kwa penalti 6-5 na wenyeji, Mashujaa kufuatia sare ya 1-1 Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.


Na kwenye Ligi Kuu hadi sasa Simba inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 46 za mechi 21, nyuma ya Azam FC yenye pointi 54 na mabingwa watetezi, Yanga wenye pointi 62 baada ya timu zote kucheza mechi 24.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad