Inawezekana Kupata Mume au mke Mzuri Kupitia Facebook?

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Katika safari ya mapenzi wanandoa huwa wanakutana katika maeneo mbalimbali, wapo wanaokutana vyuoni,shuleni, kwenye nyumba za ibada, sokoni, kwenye daladala, kuunganishwa na mtu mwingine, au baada ya kusikia sauti kwenye simu, redioni, hotelini na sasa wengine kupitia mitandao ya kijamii kama facebook

Ukweli ni kwamba katika mitandao unapoanzisha uhusiano na mtu usiyemfahamu inawezekana ameona picha yako tu nakukuambia kuwa anakupenda na wewe ukiona picha yake ukaridhika naye mkaamua kuanzisha uhusino ni vyema kuonana kabisa ili kuwa na uhakika na uhusiano mnaotaka kuanzisha  kwani unahitaji kumfahamu zaidi  na ndipo utakapoweza kufanya maamuzi ya kukubali au kukataa.

Anaweza kuwa rafiki yako wa kawaida lakini uhusiano ukaja baada ya kuonana mkafahamiana zaidi, kwani ukikurupuka na kutaka kuoana haraka haraka na yule ambaye mna chat tu kwenye mitandao unaweza kujikuta unajuta baadaye kwa maamuzi yako ni vyema kufahamiana zaidi ya kuchat ili kuwa na uhakika na maamuzi yako.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Nyangilu kamata16 April 2014 at 21:51

    Ulimwengu huu wa sayansi & tekinolojia watu wengi hasa vijana wamejikuta wametekwa na mitandao ya kijamii kwa kujihusisha na mapenzi lakini ukweli unabaki kuwa palepale mandiko yanasema tumia walau miezi 6 hadi miaka miwili kumchunguza mchumba wako siyo ukurupuke mana huko ni kuingia kinyemela/kienyeji hali hiyo husababishwa na tamaa ya mapenzi.

    ReplyDelete

Top Post Ad