FASTJET: My First and Last Experience.

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wana Jamvi,

Siku ya tarehe 26 April 2013, nilikutana na mkasa wa hawa jamaa zetu wa Fastjet na tangia siku hiyo nilinuia, kutokufikiria kutumia usafiri wa hii ndege tena. Kisa chenyewe kilikuwa hivi;

Nilisafiri kwa gari binafsi kutoka Dar kwenda Arusha tarehe 21 April 2013 na nilitarajia kurudi Dar Ijumaa ya tarehe 26 April 2013 kwa kutumia ndege ya Fastjet iliyokuwa iondoke Arusha (KIA) saa 3:30 usiku. Nilikuwa na tiketi mkononi. Taratibu za Fastjet ni kuripoti dakika 40 kabla ya muda wa ndege kuondoka. Nilikodisha taxi kutoka Arusha na nilifika KIA saa 2:40 usiku. Nilipofika, taxi iliyonipeleka pale iliondoka. Kufika mlangoni, walinzi wakanimbia kwamba nimechelewa na kwamba counter tayari imefungwa na hakuna mtu wa kunicheck in. Nilimkuta na Bwana mwingine aliyekuwa amenitangulia kufika na yeye akibembeleza kuruhusiwa kuingia. Wale walinzi walikataa katakata na ukweli ni kwamba pale counter hakukuwa na mtu hata mmoja. Kwa kushirkiana na msafiri mwenzangu niliyemkuta pale, tulianza jitihada za kutaka kuonana na mwakilishi wa Fastjet pale uwanjani. Jitihada zetu za kumwona mwakilishi wa Fastjet hatimae zilifanikiwa lakini to our suprise, yule Bwana alikuwa too arrogant kupita kiasi. Alitwambia hakuna msaada wowote anaoweza kutupatia. Ndege ilikuwa bado iko pale uwanjani. Wakati tukiendelea kumbembeleza, aliitwa kwenye radio call na hivyo akatutaka tutoke ofisini kwake na kwamba angekuja kutusikiliza baadae lakini akasema msaada pekee anaoweza kutupa ni kutukatia ticket nyingine kwa ajili ya ndege ya Jumamosi asubuhi tarehe 27 April 2013.

Baadae tulipata taarifa kwamba ndege haiwezi kuondoka kwa kuwa imepata hitilafu na kwamba abiria ambao tayari walikuwa wamepanda wameshushwa na kurudi waiting room. Yule mwakilishi wa Fastjet hakurudi tena ofisini pale ingawaje tuliendelea kumsubiri. Kwa kuwa nilikuwa na mkutano muhimu wa kuhudhuria Dar Jumamosi tarehe 27 April 2013, nilianza kufanya mpango wa kuangalia uwezekano wa kupata seat kwenye ndege ya Precision Air iliyokuwa iondoke Arusha (KIA) saa 1:55 asubuhi kuelekea Dar. Bahati nzuri nilimpata mwakilishi wa Precision Air pale uwanjani ambaye baada ya mawasiliano alinihakikishia kunipatia seat kwenye hiyo ndege. Tatizo sikuwa na cash ya kulipia hiyo ticket ambayo gharama yake ilikuwa Tshs. 195,000 one way. Baada ya kuhakikishiwa seat, nililazimika kukodisha taxi ya kunirudisha mjini ili kupata hela za kulipia ticket ya Precision kutoka kwenye ATM. Nilifanikiwa kupata hela na baada ya hapo kazi ya kutafuta hotel ikaanza. Nilipata Hotel na nililala karibu saa 6 usiku.

Saa 11:30 alfajiri tayari nilikuwa kwenye ofisi za Precision Air pale Arusha ili kupanda shuttle kwenda KIA. Kufika tu, nikaambiwa tayari shuttle ilikuwa imeondoka hivyo nalazimika kutumia usafiri wangu kwenda KIA (Ukweli ni kwamba shuttle ilikuwa haijaondoka na wala ilikuwa haijafika ila mlinzi anashirikiana na taxi drivers kudanganya abiria ili wakodishe taxi zao). Nilifanya hivyo na kufanikwa kufika Dar kwenye saa 3:45 asubuhi Jumamosi. Wakati turuka pale KIA, ile ndege ya Fastjet tuliiacha pale na sijui iliondoka saa ngapi. Abiria walilala pale uwanjani bila huduma yoyote hata maji ya kunywa hawakupewa.

Nia ya kuleta uzi huu ni kuwaambia wana Jamvi kwamba wakati mwingine rahisi ni ghali. Safari hii ilinigharimu pesa nyingi sana kwa kuwa tu nilitaka ticket rahisi ya Fastjet (Tshs. 107,000) one way lakini matokeo yake niliingia gharama zifuatazo;

1. Ticket ya Fastjet Tshs. 107,000
2. Taxi Arusha KIA x 3 Tshs. 150,000
3. Hotel tarehe 26/4 Tshs. 50,000
4. Ticket ya Precision Tshs. 195,000
Jumla Tshs. 502,000

Nilinuia hiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kujaribu kusafiri na Fastjet na ilikuwa mara ya mwisho pia. Sitakaa nithubutu kufanya makosa tena hata kama Fastjet wata improve huduma kwa wateja na kuajiri watu wanaoweza kuwasiliana kwa heshima na wateja.

Tiba

Source:Jamii Forums
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

4 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Pole sana mara nyingi makampuni Mengi huwa wanapenda kuajiri watu wasio na uzoefu ktk kazi husika hasa za hapa nyumbani, ilimradi wasitumie fedha nyingi ktk kuwalipa,ndiyo mana kuujuwana na undugu umekuwa mwinga sana. Na wao bila kujua ni kwakiasi gani ataiathiri kampuni,Kama hivi kwasasa siyo wewe tu kutotumia hizo ndege tena watu wanajua sasa how weak they are!.wanatutia aibu sana hawa sasa hapo angeluwa mzungu Wala lisingetokea.

    ReplyDelete
  2. Kiukweli hata mimi ilishanitokea mkasa unaofanana na huo kwa ndege ya fastjet! hawana na hawajui customer service. mteja kwao ni bwege! Mara elfu 10 precision

    ReplyDelete
  3. Da pole sana kwakuspend a lot of cash,sio ubinadamu kabsaa

    ReplyDelete
  4. Hao FastJet kwanza ndege yao mbovu ilishatugomea kuruka mara kadhaa.Sio ndege customer service yao 0 .pole sana mdau kwa yaliyo kukuta.
    We learn through mistake don't go there again!!!

    ReplyDelete

Top Post Ad