AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
“Madhumuni ya kutoa single hii ni kuwakilisha Tanzania na muziki wetu Africa na dunia, na pia nchi zenye kupendelea kuangalia Big Brother ambao wafuatiliaji wa kipindi hicho cha miezi mitatu wako zaidi ya million 20, amesema Julio kwenye maelezo yake.
“Huu ndo muda nchi yetu itasikika kirahisi kimuziki kwa nchi 54 Africa kwasababu ya nyimbo kuwa kali na vigezo vyote na kwamba inahusiana na hiyo show. Wimbo unaitwa MR BIGB ROTHER na unaoongelea Big Brother kama show,nchi zinazoshiriki,msiba tuliopata mwaka jana heshima kutoka kwa watanzania baada ya kumpoteza mshiriki mkubwa mwaka jana Goldie,” amesisitiza Julio.
“Huu ndio mwimbo wetu kwa mara ya kwanza katika historia ya bigbrother msanii kutoka nchini kutoa mwimbo kwa ajili ya Big brother Africa na support ya watanzania itatufanya kufikisha muziki wetu nje ya Tanzania na Africa. Big Brother mwaka huu inaanza baada ya wiki mbili, 26 May. Tujivunie cha kwetu na kupeperusha bendera yetu Africa.”
Ngoma hii imetayarishwa na Timewreckordz na NK Production.Mpaka sasa Julio ameshafanya ngoma na wasanii kama Chege, Matonya, Cassim, Countryboy,Chidi Benz, Ukeme, Bskillz,Lamar,Lucci da don,Jokate,ROBZ na wengine.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK