Kibadeni Sasa Rasmi Simba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kocha Abdallah ‘King’ Kibadeni anaanza kazi rasmi Simba kesho ya kuinoa Simba kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara na mashindano yajayo ya Kombe la Kagame.
Akizungumzia kuhusu kutua kwa Kibadeni katika klabu ya Simba, Kaimu Makamu wa klabu hiyo, Joseph Itang’ale alisema mkataba rasmi bado hawajasaini na Kibadeni ila wanatarajia kumpa mkataba wa miaka miwili au wa mwaka mmoja.
Kuhusu wana malengo gani na Kibadeni, Makamu huyo alisema Kibadeni ndiye kocha pekee ambaye ameshawapa ubingwa Simba mara tatu na alijenga timu ya vijana ya Simba ambayo mpaka sasa inafanya vizuri.
Akizungumzia kwa nini wameamua kuachana na kocha Patrick Liewig raia wa Ufaransa, Makamu huyo wa Simba alisema kocha Liewig alikuwa akibagua watu ndani ya klabu ya Simba na kujiona yeye ndiye yeye jambo ambalo lilikuwa likiwakera wachezaji, pia hajafanya kazi yake vizuri katika kukinoa kikosi cha Simba.
Itang’ale alisema Simba wataanza mazoezi yao kesho kwenye uwanja wa Kinesi, Dar es Salaam kwa ajili ya kujiandaa na mashindano ya Kagame, ambapo kikosi chao kitakuwa chini ya Kibadeni.
‘’Tumemkabidhi mikoba yote Kibadeni na tumekubaliana naye kila kitu na kesho ‘leo’ kocha huyo atakutana na kamati zote za ufundi kwa ajili ya kueleza programu nzima tayari kwa kuanza kazi,’’ alisema Itang’ale.
Pia Itang’ale alisema kuwa tayari wamemalizana na kocha Liewig kwa amani na sasa wameamua kujenga Simba mpya kwa ajili ya mashindano mbalimbali yaliyopo mbele yao.
Hata hivyo, kocha Kibadeni alipotafutwa na gazeti hili kuzungumzia kutua klabu ya Simba alisema kuwa msimamo wake kama ataendelea kuwa na Kagera Sugar au atajiunga na Simba utajulikana wiki ijayo ambapo atatoa msimamo wake.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad