AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kwa mujibu wa DJ Fetty, habari zenye uhakika zilizotoka kwa Dr aliekuwa ICU, katika hospitali ya St Hellen Joseph, zimethibitisha kuwa msanii aliekuwa na Ngwea wakati mauti yanamkuta, ambae yeye pia alikua hoi hospitali, anaendelea vizuri, na anaongea kwa sasa, ila uchunguzi wa kile kilichosababisha kufikishwa hospitali hapo bado unaoendelea.
M2 the P alipelekwa katika hospitali ya St. Hellen iliyopo nchini humo kwa matibabu baada ya kukutwa amepoteza fahamu akiwa na Mangwair aliyefariki dunia jana. Mwili wa marehemu Mangwair bado upo katika hospitali ya St. Hellen na mipango ya kuhamisha mwili huo bado inaendelea.
Baadhi ya Watanzania waishio nchini Afrika Kusini wamejikusanya kwa ajili ya kuandaa mipango ya kuhifadhi mwili huo pamoja na safari ya kuuleta nchini Tanzania.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK