Topic: Arusha: Aliyerusha bomu alikuwa kavaa kanzu nyeupe na koti la Mvua la Kahawia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ilivyokuwa

Watu walioshuhudia tukio hilo wanasimulia kuwa bomu hilo lilirushwa yapata saa nne asubuhi wakati mgeni rasmi akijiandaa kufungua jengo la kanisa baada ya ujenzi wake kukamilika.

Kamanda Sabas alisema mtu aliyerusha bomu hilo alitokea nyuma ya kanisa hilo la ghorofa na kurusha bomu hilo kwa mkono wa kulia... “Alifanya jitihada za kupenya ili awafikie viongozi lakini alishindwa kutokana na wingi wa waumini waliokuwapo kwenye eneo hilo.”

Msemaji wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Arusha, Padri Festus Mangwangi alisema aliyerusha bomu hilo alishuhudiwa na mtoto mdogo aliyekuwapo kanisani hapo.

“Kwa mujibu wa maelezo ya mtoto huyo, mtu huyo alikuwa amevaa kanzu nyeupe pamoja na koti la mvua lenye rangi ya kahawia na alikimbia mara baada ya kulirusha katikati ya watu. Ametusimulia kuwa mtu huyo baada ya kurusha bomu lile alikimbia na kuwahadaa watu kwa kuita ‘mwizi mwizi mwizi…’ akionyesha mbele kama kuna mtu anayemfukuza jambo lililowazubaisha watu lakini mtoto aliyemwona akirusha bomu aliwaeleza kuwa ndiye mhusika.”

Akizungumzia tukio hilo, Ndowe ambaye amelazwa Mount Metu, alisema aliona kitu kikidondoka kanisani na kutoa kishindo kikubwa na watu kuanza kukimbia ovyo. Alipoteza fahamu kutokana na kutokwa na damu nyingi.

Debora ambaye ni Polisi alisema alipoona kitu kikidondoka alibaini mara moja kuwa ni bomu. Alijeruhiwa mguu na mkono. Elizabeth alisema aliona kitu kama kibuyu kikianguka chini na kupasuka na baada ya hapo hakujua kilichoendelea.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad