TUNDU LISSU ADAI HATI ILIYOPELEKWA BUNGENI NI FEKI

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Dodoma. Hata baada ya Wajumbe wa Bunge Maalumu kugawiwa nakala za Hati ya Muungano, Tundu Lissu, ameendelea kung’ang’ana kuwa haipo, ni feki.

Akizungumza kwenye Viwanja vya Bunge mjini hapa mara baada ya nakala kugawiwa bungeni, Lissu ambaye aliibua hoja hiyo alisema; “Hivi hawa wanamghiribu nani? Nasema hiyo hati haikuwahi hata kupelekwa Umoja wa Mataifa.”

Alisema saini iliyo kwenye hati hiyo ni tofauti na zilizo kwenye hati ya Mabadiliko ya Kwanza ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya 10 ya Juni 1965, Hati ya Muswada wa Sheria ya Udhibiti wa Fedha za kigeni na Sheria ya kugawa ardhi kwa Wazanzibari ambazo zote zinafanana.

Lissu alisema kwa miaka 50 haikuwahi kuonyeshwa, wala haikuwahi kuwa UN na hata Zanzibar hawana. Alisema walishuhudia Benard Membe (Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa) akisema iko UN, jambo alilosema ni kudanganyana tu.

Alisema nyaraka kama hizo, mkataba wa Uhuru zinatakiwa kuwekwa Makumbusho ya Taifa kwa kuwa ni nyaraka wazi zinazotakiwa kuona na kila anayetaka, kwa rahisi.

“Marekani ilipata uhuru zaidi ya miaka 200, lakini kila nyaraka za uhuru zinaonekana kwa rahisi siyo hapa...mambo yanafanyika chini kwa chini, utadhani biashara haramu,” alisema.

Baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu wamembeza Lissu kwa hoja hiyo wakisema hatua ya nakala zake kufikishwa bungeni ni sawa na kumfunga bao la kisigino na kuhoji watazungumza nini baada ya hati kupatikana.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

13 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. lisu tushachoka na siasa zako wewe hukubali kushindwa usituchanganye shuhulikia vitu vyengine hili umeshindwa

    ReplyDelete
  2. Huyu tundu lissu inafaa akamatwe atandikwe bakora maana yeye ndio anaechochea mipangilio pumbavu zake

    ReplyDelete
  3. Huyu nae kuma kweli,kila kitu ye anapinga tu

    ReplyDelete
  4. wewe mdau 2:52 acha kabisa matusi... kwani kuhoji ni zambi? hata haki zenu hamzijui, mmelelewa vibaya na baba enu wa taifa, hakutaka chohote kihojiwe hata pumba. Je? unaweza thibitisha uhalali hiyo hati. Mbona haikupatikana ilipoihitajika? Ikiwa ni mpenzi wa YANGA usisifie tu YANGA hata wakifanya makosa, wataangamia bora waambie ukweli wajirekebishe. Unapoomba kazi unaambatanisha kivuli cha cheti na ukiitwa kwenye mahojiano unatakiwa uende na cheti halisi ili kuthibitisha.. Lisu na watanzania wenye IQ makini wangependa kuthibitisha hati hiyo siyo kukubali tu kama mazuzu.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hapo umenena na umefafanua kisomi na kiakil zaidi!kuna mijitu mingine upeo wa kufikiri ni mdogo ndio haya yanayosababisha upatikanaji wa maviongozi mburula bungeni kama hili li Mwigulu mchembu hii yote ni sababu ya wananchi mbulura wa kufikili.

      Delete
  5. Haipelekw basi hiyo original na sio kupinga kupinga tu

    ReplyDelete
  6. Unaona watu wanatukana baada ya kujenga hoja!ndoo ujue weledi Wa few tanzanian!mtu ampinge lisu kwa hoja dhidi ya kule anachosema si matusi,kutukana ni kuonyesha kutoelewa hoja ya lisu.napenda sana tubishane kwa hoja ili wengi wetu tusiojua mengi tujifunze.

    ReplyDelete
  7. lisu hana hoja kataka hati kishaiona bado anasema batili sasa ana manamaanisha kitu gani au apate jibu gani tena yeye kahoji kwa mdomo na tena kujipa uhakika kajibiwa kivitendo bado anabisha na nyinyi mnamuamini duh mapenzi gani haya unamkuta mkeo kalala na jamaa kwa macho yako yeye anakuambia hajalala bado unamuamini tuache ujinga tundu lisu nae nakosea kwani na yeye binadamu tutambue yeye hawezi kuikubali ile hati hata kidogo kwa sababu alijenga hoja ambayo alijipa uhakika na kutoa mifano na akina nyinyi mkamkubali kua muungano haukua na hati inachekesha mfunge mkataba kwa mdomo yeye yeye kipindi cha nyuma anasema makubaliano ya hati ya muungano ili kua hivi au hivi katika bunge la katiba kaja kivengine anasema haipo huu ni ubabaifu alikua anaitaja makubaliano ya hati katika bunge la jamuhuri ya tanzania katika bunge la katiba anasema haipo huyu hawezi kuikubali hata kidogo akiikubali hadhi yake itashuka kwa watu watamtambua kuwa huwa nasema uongo ili atetee hoja zake.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Na wewe una uhakika gani kama ni yenyewe?au ndio mahaba niue ccm?

      Delete
  8. kweli libisu tumelichoka

    ReplyDelete
    Replies
    1. Wewe nawe unamapengo nini "libisu"ndio nini sasa.

      Delete
    2. Nimechoshwa na jinsi nchi ilivyo sasa kila mtu anasema analojickia

      Delete
  9. Tundu la mkundu ni kwa ajili ya kunyea tu sio kuongea

    ReplyDelete

Top Post Ad