Dk.Mengi na Patrick Ngowi Waibuka na Tuzo za Wafanya Biashara Bora Africa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk. Reginald Mengi, ameibuka mshindi wa tuzo mbili kwenye fainali ya shindano la kuwania Tuzo ya Mwaka ya Mfanyabiashara Bora Afrika (AABLA) kundi la Afrika Mashariki.

Sherehe za kutoa tuzo hizo zilifanyika jijini Nairobi, Kenya Jumamosi iliyopita.

Dk. Mengi alitunukiwa Tuzo ya Mfanyabiashara Bora Afrika kwa mwaka 2014, kutoka kundi la Afrika Mashariki. Majaji wa shindano hilo pia waliamua kumtunuku Tuzo ya Maisha ya Mafanikio kwa kuongoza katika suala la uwajibikaji kwa jamii.

Dk. Mengi ambaye pia liingia kwenye kurasa za gazeti maarufu la Forbes Africa la Julai mwaka huu wa 2014, amekuwa akichangia sehemu kubwa ya muda na rasilimali zake kwa ajili ya kufadhili kazi zinazogusa maisha ya jamii.

Kwa upande wa Tuzo ya Kijana Mfanyabiashara Kiongozi wa Mwaka, tuzo hiyo ilienda kwa Patrick Ngowi, CEO wa Helvetic Solar anayeongoza kampuni inayokua kwa kasi kwenye mtandao wa nishati mbadala katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Anaongoza wafanyakazi zaidi ya 300, akichangia kwenye ukuaji na maendeleo yanayolenga mipango ya kibiashara katika taifa la Tanzania na ukanda mzima wa eneo hili.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad