AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hayo yanakuja siku chache baada ya Wema aliyewahi kuwa mchumba wa Kanumba kudai kusumbuliwa na tatizo la kukosa uwezo wa kuzaa hivyo mzee huyo kujiongeza na kusema ni kwa sababu alitoa mimba ya mwanaye huyo.
Akizungumza na waandishi wetu, baba huyo alisema kama kweli Wema alitoa mimba ya Kanumba basi atakuwa alijilaani kwa sababu ukoo wao ukitoa mimba unaweza kufa au kujilaani (kutokupata mtoto) hivyo anatakiwa kutambika kwa kulala juu ya kaburi la mama mkubwa wa Kanumba ambaye ni bibi wa babu wa mzee Kanumba.
Alisema sambamba na hilo, Wema atatakiwa kurithiwa na ndugu wa Kanumba (kati ya kaka au mdogo wake).
“Kwenye ukoo wetu ukitoa mimba kuna mambo mawili, moja ni kufariki dunia au ‘kujikila’ (kujilaani) kwa kutokuzaa, pengine ndicho kilichomtokea Wema,’’ alisema baba Kanumba.
Mzee huyo alisema kuwa mama mkubwa huyo alishafariki dunia kwa hiyo yeye na marehemu Kanumba walipaswa kwenda kaburini kwake kufanya tambiko zito, wakiwa wamevaa mavazi maalumu ya kiasili na mikononi wameshika vibuyu, jambo ambalo lingempasa Wema kukaza moyo.
Alisema kuwa wakiwa kaburini hapo, Wema alitakiwa achotewe mchanga na kushikishwa kisha kusemewa maneno ya kuomba msamaha kwa kilichotokea.
Alisema walitakiwa waende na maziwa, unga wa mtama na hayo mavazi maalumu kwa ajili ya tambiko hilo.
Aliendelea kudadavua kwamba, kwa sasa Kanumba hayupo duniani hivyo Wema anapaswa kuchukuliwa na kaka au mdogo wake wa damu kwenda kutambika, ikiwa ni pamoja na kuzaa naye ili kufungua mlango wa kizazi, hata kama ataachika basi ataendelea kupata watoto.
Baba Kanumba alisema mama mkubwa huyo ni bibi yake mzee Charles Kanumba ambaye katika ukoo wao alikuwa mganga wa wanawake walioshindwa kupata watoto au wenye tatizo la kizazi.
Hata hivyo, baba Kanumba alimalizia kwa kusema kuwa, ingekuwa zamani ilikuwa ni kurithiwa tu lakini kwa sasa mila hizo zinapingwa vikali.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Huo ni ujinga na ushirikina wa hali ya juu,,, Bi Wema consult the doctors instead!!!
ReplyDeleteAache tu kunywa pombe kabisa halafu aone kama kiboro hakijamkatikia
ReplyDeleteUpuuzi mtupu, wanawake kibao washatoa mimba na kuzaa wamezaa bila shida, aseme tu anamtaka binti wa watu akamkoromee. Wema anaweza sana kuzaa ila aliamua tu kusema hazai ili apunguze kelele za Waswazi waliokuwa wanamuandama kumuuliza atazaa lini na kwanini hajazaa mpaka leo. She just decided to shut their big mouths and she succeeded.
ReplyDeleteAtarithiwa vipi wakati hakuwa mke wa kanumba??? Hayo mambo ya tambiko ni ushirikina mtupu Mungu peke yake ndo anatowa mtoto
ReplyDeletehuyu mzee anamambo ya kishirikina sana, hata hao wanaume wa lulu wanaokufa hasa huyu wa juzi usikute anamiguu yake. yani sijui anawazaje vitu vyake
ReplyDelete