AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
K-Lynn ameiambia Bongo5 kuwa maisha akiwa kama mama watoto wawili mapacha yamekuwa ya aina yake na anayafurahia kila sekunde.
“Nimejifunza kuwa mvumilivu, nimejifunza upendo ambao sijawahi kujisikia kabla. Jinsi unavyompenda mtoto ni tofauti ambavyo unaweza kumpenda mtu yoyote yule katika maisha yako,” alisema.
Katika hatua nyingine Miss Tanzania huyo wa zamani alisema hakuna uwezekano wowote wa yeye kurejea tena kwenye muziki.
“Kwa bahati nzuri sana baada ya kufanya uamuzi wa kutokuwa kwenye muziki, niliweza kupata kitu kingine ambacho kimeuteka moyo wangu. Kufanya interior design kunanifurahisha kuliko hata muziki.
"Nafurahi sana kujua kwamba kuna watu wangependa kunisikia ama kusikia nikiimba lakini nafikiri moyo wangu umehamia kwenye sanaa nyingine.”
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Love you K-lyin
ReplyDelete