Mjue Body Guard wa Mwanamuziki Diamond -Kumbe ni Komandoo wa Kuogopwa Hasa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Bodigadi wa Diamond Mwarabu Seleman Mirundi akifanya mazoezi ya kikomandoo kwenye msitu wa chuo kikuu kuhofia watu wasione mazoezi yake.

Juu picha za wanajeshi wa Irani ambao pia ni makomandoo ambao awefanyanao mazoezi.
Hapa akiwajibika kumlinda boss wake nchini Burundi.

Mwarabu Seleman Mirundi akiwa nchini Iran hivi karibuni alipokwenda kwa mara ya kwanza kushiriki michezo ya mapigano ya hatari ambayo hufanywa na wanajeshi hasa walifuvu ukomandoo. Mwarabu Seleman Mirundi akiwa nyuma ya bendera ya Tanzania tayari kupambana na Komandoo wa Iran ambae hata hivyo alimchakaza vibaya na kuokolewa raundi ya kwanza
Hiki ni cheti alichotunukiwa nchini Iraq baada ya kumsambaratisha Komandoo wa nchi hiyo ambae hakumtaja jina. Hiki pia cheti alichotunukiwa na nchini Mozambique baada ya kuwatandika wanajeshi kadhaa nchini humomaskanibongotz Mwarabu akifanya mazoezi mepesi na mmoja wa maofisa usalama wa nchini Tanzania .

Jamaa huyu hakuwa anafahamika sana hata kwenye matamasha mbalimbali ulikuwa huwezi kumkuta lakini baada ya kupata kazi ya kumlinda staa wa Bongo Flava nchini Naseeb Abdul Diamond alianza kujulikana zaidi huku watu wakimchukulia kama mtu wa kawaida sana kama mabaunsa wengine.

Jina lake halisi anaitwa Mwarabu Suleiman Mirundi huyu baada ya kupata taarifa za kuwa huyu jamaa si mtu wa kawaida kwenye jamii ilifanyajitihada za kumtafuta huku kupatikana kwake huwa ni kwa nadra sana huwezi kumkuta mitaani kama tuwaonavyo mabaunsa wengine wanazurura mitaani. baada ya kutonywa sehemu anapoweza kupatikana kijana huyo ambapo ni msitu wa chuo kikuu ndiko anakofanyia mazoezi mara nyingi akiwa na mwanamuziki na bondia Zora D ndipo nilipofunga safari hadi huko na kumkuta kijana huyo akifanya mazoezi ya hatari kuyaona. Mwarabu alianza kuelezea ingawa hakupenda watu wajue kama yeye ni mtu wa aina hiyo lakini alianza kufunguka kama ifuatavyo " Dada mimi ni Komandoo lakini sio wa JWTZ hapana nimefuvu mazoezi haya ya mapigano nchini Iran toka mwaka 2010 baada ya kwenda kule kuchgeza mchezo wa kutumia mabavu ndipo niliposhinda kwa kumchakaza vibaya Komandoo wa Iran" Alisema Mwarabu Baada ya hapo Jeshi la nchi hiyo baada ya kumuona sio mtu wa kawaida kuwa raia wa kawaida ndipo alipochukuliwa Kambini humo kwa ajir ya kufanya mazoezi hayo ya hatari duniani hadi mwaka juzi 2013 ndipo walipompatia cheti cha kuhitimu kama kinavyoonekana pichani.

Hata hivyo Mwarabu anasema kwa jinsi alivyo na mazoezi aliyoyapata chini ya watu kumi hatakiwi kupigana nao hata wakija na shoka isipokuwa zaidi ya hapo ndipo kidogo atawapiga makofi tu na kuwaacha lakini sio aseme atoe kichapo kwani pigo lake moja mtu anabadilishwa jina mara moja na kuitwa marehemu. Mwarabu ambae kwa sasa ameajiriwa na mwanamuziki Diamond na analipwa mshara mnono kwa kazi ya kumlinda ambapo hadi sasa amenunua viwanja kadhaa na ujenzi unaendelea na si nyumba za kitoto huku akiwa na usafari zaidi ya gari tatu ambapo moja boss wake alimnunulia na mbili amenunua kwa mshahara anaomlipa na hadi sasa anakafikisha kilo 190 wastani wa kilo 200.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

9 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Komandoo gani huyu unaemsifia hata bastola hana,,ni misuli tu katunisha kifua basi zaidi ya hapo ukomaandoo anaosifika nao hana,Kama angelikuwa komandoo asingeajiliwa na Domo kwa mshahara mbuzi (toilet paper) angelikuwa analipwa kwa dola somewhere some place..Hacheni kumsifia hivyo na huko Iran hajawai kushiriki hayo mashindano ya kikomandoo na wala hakuna mashindano kama hayo,,huyu ni baunsa wa mitaani aliyepata bahati ya kuajiliwa na Domo,zaidi ya hapo hana lolote.Komandoo utawaona movement zao>>> huyu ni komandoo wa mitaani tandale.We mwandishi unasifia ujinga

    ReplyDelete
    Replies
    1. Tang lin wabongo mlikubal chenu dharau zmewazid ndo maana amfanikiw et toiletpaper

      Delete
    2. Acha UPUMBAVU wewe mwehu, na lini komandoo akategemea bastola??? unataka mpaka atembee kainua bastola juu ndo uamini?? Nyaaaambaf kabisa

      Delete
  2. Na wewe adimin umekosa cha kuonge a

    ReplyDelete
  3. Komandoo wa uswahilini,

    ReplyDelete
  4. Habari zenu za kucopy na kupaste zinachosha nyie watu, hao wairani na hicho cheti na bendera ya tz viko wapi...... my foot!!

    ReplyDelete
  5. Anyway hongera zake... wamechukuana kishkaji wala haikuwa big deal kumpata coz mtu wa kitaa tandale mjomba huyo. Na sio tu mshahara mnono jamaa anapiga issue zake zngine binafsi na anajituma. Jamaa peace na very respect. Wewe admin tu unaleta utumbo wako na stori yako isikuwa na mbele wala nyuma..... jitume kutafuta habari kamili kwa kina na za ukweli. Sio mambo ya copy and paste.... jinga sana wewe!

    ReplyDelete
  6. Adimin fala tu! Unatunga story tupende blog yako! Acha hzo mambo, eleza ukwel nasio mbwembwe

    ReplyDelete
  7. mbona sijaona cheti wala picha unazo sema?

    ReplyDelete

Top Post Ad