Lowassa AFUNIKA Iringa.....Maelfu Wahudhuria Mkutano wake, Awataka Wafuasi wake Wazilinde Kura Zisiibiwe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa amesema amechoshwa na manyanyaso wanayoendelea kuyapata wakulima hapa nchi kwa kukopwa mazao yao na kutozwa ushuru na serilkali bila ya wao kupata faida yoyote.


Lowassa alisema punde atakapochaguliwa kuongaza nchi kitu kikubwa atakachokifanya kuwasaidia wakulima ni kufuta ushuru wote wa mazao kuhakikisha wakulima wananufaika na jasho wanalolitoa wakati wa kilimo.



Lowasa ameyasema hayo leo wilayani Mufindi alipofanya mkutano wa hadhara wa kampeni katika Uwanja wa Shule ya Msingi Wambi, mjini Mafinga.



Lowassa alisema watu wamekuwa wakizungumza kuwa CCM ni wezi wa kura kwasababu ni wajanja sana katika kufanya michezo michafu katika chaguzi na maneno hayo si yakuyabeza wala kuyafumbia macho.



“Mimi nataka kila mtu akihifazi vizuri kichinjio chake (kadi ya kupigia kura) na siku ya kupiga kura ikifika nawaomba wanawake na wanaume wajitokeze kwenda kupiga kura ila wakina baba nawaomba mkishapiga kura fanyeni kazi ya kuzilinda kura zenu” alisema Lowassa



Katika mkutano huo, waziri wa zamani wa Elimu, Joseph Mungai alipanda jukwaani na kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mafinga Mjini kupitia Chadema, William Mungai ambaye ni mtoto wake.



Mungai aliwahi kuwa mbunge kwa miaka 35 kupitia CCM na aliweza kuteuliwa nafasi mbalimbali za uwaziri ikiwamo Wizara ya Kilimo, Mambo ya Ndani na Wizara ya Elimu.



Mungai alisema wananchi wa jimbo hilo wanatakiwa kumchagua William Mungai kwa sababu mbunge aliyemaliza muda wake katika jimbo hilo hakuweza kuongoza kama alivyofanya yeye.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

7 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Wacheni uwongo mbona picha hio ni ya jangwani sio ya Iringa soma gazeti la mwananchi msema kweli mtajidanganya sana hukumu tarehe 25 October picha za mafuriko ya Jangwani tutadanganyiwa kila mkoa na hampati kitu CCM oyeeeeeeeeeeeeeee Magufuli hana mpinzani mtatukana sana mpaka kumekucha

    ReplyDelete
  2. Hata picha ikiwa ya jangwani lakini si ukawa

    ReplyDelete
  3. Poleeee yako weeeee mwanzo mlisema tuna edit Leo za jangwaniboooh tunakodi wstu oooh tunahonga watu msijiongeze kalieni umbea na unafki ndio man's Sera senu zimejaa matusi na masengenyo na mauwongo Yale Yale ya miaka 52 iliyo pita nothing new kenge wewe Wa ccm apo ulipo unamachacha kibao bado tu unagandia ccm matako yako kama ya sisizimizi nyangau nyama pori mkubwa wewe mwaka huu ndio tutaliona I'll bao lenu la kisigino letu la kwapa upon hapo

    ReplyDelete
  4. Haaaaaa CCM mpoooooooo,,,,,,,,ngoja niamshe popo mvua ya natusi itakavyo ni nyeshea,,,,,,,,UKAWA MPOOOOOO,,,,,,,TUTAONANA OCTOBER 26,,,,,,MKIAPISHWA,,,,,,KILA MKULIMA LAZIMA TUMPE TRECTA,,,,CHEZEA LOWASAA WEWEEE,,,,,,,

    ReplyDelete
  5. na bado......na bado....oooo........badooooo...mtasoma namba!!

    ReplyDelete
  6. LOWASSA MAANA YAKE NI USHINDI MKUBWA.TULIKUWEPO KWENYE MKUTANO WAKE HUU MKUBWA WA KAMPENI MJINI IRINGA YAANI NI RAHA TUPU WAHUDHRIAJI TULIKUA KWA MALAKI PALE KIPO KITU KIPYA TULIPATA KUMBE LILE SAKATA LA PESA ZA ESCROW FUKO KUBWA LA BILLION TANO LILIKWENDA KWA MHESHIMIWA KIKWETE AMBAYE NDIYE ALIYEMWAGIZA GAVANA WA BENKI KUU DR.NDULLU ATOE PESA HIZO.NI HIVI RAIA WENZANGU MHE KIKWETE ALIYEBAKIZA SASA MWEZI NA USHEE KUITAWALA NCHI NI LAZIMA AJE AKAMATWE AFIKISHWE MAHAKAMANI KWA WIZI NA MATUMIZI OVU YA OFISI INAYOPASWA KUHESHIMIKA SANA.YAPO PIA MENGI MENGI MHESHIMIWA SUMAYE AMETUFUNGUA MASIKIO HAPA IRINGA.TUNA WASIWASI HALALI SASA KUA HUENDA KIKWETE NA FAMILI YAKE WAKAKIMBIA NCHI BAADA YA HUU UCHAGUZI MKUU OCTOBA 25,2015 ITABIDI SASA NYENENDO ZAKE ZIANZE KURATIBIWA

    ReplyDelete
  7. Ata aibu huna eti ccm oyeeee!!hospital hazina madawa,shule hazina madawati,mishahara ya walimu,police,madaktari,manesi ni duni.Kweli mmepewa limbwata na CCM,wala hamjielewi.pambavu!!

    ReplyDelete

Top Post Ad