'Rais Magufuli Ndiye Rais wa Kwanza Duniani Kuwa na Asilimia 96%' Lemutuz

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kwa Mujibu wa Gallup Polls by British Institute of Public Opinion iliyofanywa Mwezi uliopita the FACT is utafiiti wao wa kisayansi unaonyesha katika Mwaka wake mmoja madarakani Rais Magufuli amefanikiwa kukubalika sana na Wananchi kwa 96%, utafiti ulifanywa kwa kutumia Mobile Survey through Wananchi 1,813.

- Kwa mujibu wa matokeo hayo Rais Magufuli, amefanikiwa kufanya yafuatayo kwa ufanisi unaokubalika na Wananchi wengi:- (1). Kuishinda Rushwa 75%, (2). TRA sasa ipo on the right track 85%, (3). Education has improved by 75%, (4). Mahakama zetu sasa zipo mstari unaotakiwa kwa 73%, (5). Afya improved by 72%, (6). Maji Safi kwa Wananchi 67%, na kubwa kuliko zote ni Wafanyakazi Serikalini na Mashirika yake sasa wamekuwa 95% kwa Accountability na Fast Response.

- Now Rais Magufuli sio Malaika, na sio siri kwamba Wananchi wote tulikubaliana kwenye uchaguzi uliopita kwamba Taifa letu lilihitaji mabadiliko na tulihitaji kumchagua Rais wa kutuletea mabadiliko, matatizo yetu makubwa ya Taifa siku zote yamekuwa ni Respect to the Rule of Law na Uchumi Mwalimu Baba wa Taifa the greatest ever alikuwa na mapungufu kwenye hizo two lines na zimetusumbua kwa muda mrefu sana hili taifa ni only now Rais Magufuli ameanza kuyatafutia ufumbuzi na matokeo yameanza kuonekana.

- Wananchi wengi hapa Mjini sasa hawana tena pesa za kuchezea kama zamani ambapo ilikuwa kawaidaa kukuta Kijana mdogo akiendesha gari la kifahari na akiwa na mabunda ya Mamilioni ya pesa kwenye gari lake, kuna Vijana hapa mjini walikuwa wakitengewa meza zao kwenye Vilabu vya starehe yaani haruhusiwi kugusa mtu kwa sababu wanatumia pesa nyingi sana wanapokwenda pale, Mikutano ya Bodi za Wakurugenzi wetu mingine ilifikia mpaka kufanyika Johannesburg, au Singapore ambapo wajumbe wa bodi waliruhusiwa kwenda na familia zao, Bandari yetu ilikuwa unakusanya Billioni 40 tu kwa mwezi badala ya Tsh. Billioni 300, na mengineyo mengi ambayo yalisababisha Taifa letu kuwa na tabaka fulani la wachache wenye pesa na wengi Masikini, katika Mwaka mmoja wa Rais Magufuli tumejionea mabadiliko makubwa sana na kwa mara ya kwanza katika historia ya Taifa letu wale walioitwa Vigogo au the untouchables sasa wapo Rumande Keko wanasubiri kesi zao.

- I understand that baada ya kuona hawana upenyo wa kuingilia au kutokea kwenye mfumo mpya wa sasa zaidi ya kutakiwa kufanya kazi zao kwa mistari ya Kisheria, Wapinzani wameamua kutumia Social Media na hasa Media kwa ujumla kumshambulia sana Rais Magufuli, kuna pahali wameanza hata kumsifia Rais JK kwamba ni bora zaidi, lakini hatujawasahu hawa ndugu zetu na tabia yao ya kubadilika badilika kama Kinyonga wakifuatia masilahi yao aidha ya Vyama vyao au binafsi, Waliwahi kutuambia kwamba CUF ni Chama cha Mashoga lakini walipotaka Umoja wa UKAWA wakajiunga nao, Waliwahi kumshambulia sana Waziri Mkuu Mstaafu Lowassa mpaka walienda mbali sana na kutaka apigwe Risasi hadharani kwa Ufisadi, leo wamebadilika kwamba Ushahidi upo wapi kwa sababu amejiunga nao,

- Infact wameanzisha hoja moja dhaifu sana kwamba mbona Rais JK alikuwa anawaita Wapinzania na kuwasikiliza ushauri wao kwenye uongozi, sasa tunatakiwa kuwauliza kwamba mlikuwa mnamshauri Rais JK on what lines na huku wote tunakubaliana kwamba Taifa lilikuwa limeoza? Rais Magufuli awasikilize nini hasa kizuri mlichowahi kulifanyia Taifa hili huko nyuma? The Americans wanasema kama kuna Kiongozi mahali ameoza basi ni system nzima so kama as a nation tulikubaliana kwa kauli moja kwamba tunataka mabadiliko basi iilikuwa na maana kwamba 360 Degrees U turn ambayo ndio tunayoyapitia sasa yaani total mabadiliko, ninawaomba huko upande wa pili muwacheni Rais afanye aliyoyaahidi kwenye kampeni zake za kuomba Urais na Ilani ya CCM, subirini Mwaka 2020 kwenye uchaguzi unaofuata kwa sasa uchaguzi umekwisha.

- MUNGU IBARIKI TANZANIA!!

Le Mutuz Nation
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

13 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Lemutuz,

    Nikiri hapa wazi hadharani na nipende kuamini kwamba kwa maelezo yako haya yanayotokana na utafiti hata bila ya utafiti, umekonga nyoyo za watanzania wengi sana pengine asilimia 98, (2% wapinzani).
    Ni ukweli ulio dhahiri na msema kweli mpenzi wa Mungu. Watu wenye akili na busara zao, ndani na nje ya nchi wanakiri kwa macho na vinywa vyao kwamba Rais John Pombe Joseph Magufuli ni rais kati ya marais anayestahiki. Lakini utashangaa kuwaona watu wachache sana waliofilisika kifikra wakithubutu bila aibu kubeza juhudi maridhawa, mujarabu za Mheshimiwa Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli. Ama kweli nabii hakubaliki nyumbani kwao.
    Hiyo si hoja, hoja ni kwamba tumempata rais bora tumtie moyo kwa kushirikiana naye kujiletea maendeleo.

    ReplyDelete
  2. Kunywa upendavyo,kula upendavyo hapo kwa mangi Le-mutuz,nakuja kulipa.

    ReplyDelete
  3. YAANI JAMANI!NI KUMSHUKURU MUNGU TU KUTUPA JPJM.

    ReplyDelete
  4. Ninachokijua-
    .Ukiona mtu hamuungi mkono JPJM,basi ni
    1.fisadi,au baba/mama/mke/mume wake alikuwa fisadi.
    2.Mvivu na kwamba alitegemea kula/kuhongwa kwa mgongo wa mafisadi
    3.Anatoka kazkazini na asiyejitambua.
    4.Team mabadiliko ya kuzungusha mikono,ili mradi tu kashabikia.
    5.Alikuwa kwenye nafasi ya kula vya umma na sasa katumbuliwa.
    6.Ni mgonjwa amekata tamaa ya kuishi anatamani UKUTA tumwage damu.
    7.Alizoea kutoa amri kwa wanyonge hata kama yeye ndio ana makosa.
    8.Kashika rasilimali za umma na sasa tumbo joto.
    9.Alizoea/alipenda kuingia kazini kwa muda aupendao yeye.
    10.Alitegemea JPJM atampa cheo imekuwa ndivyo sivyo.NA (.......)
    hata mimi nilikuwa na matatu kati ya hayo ila sitaki unafiki,
    kwa sasa namkubali JPJM.
    MUNGU IBARIKI TANZANIA.

    ReplyDelete
  5. Mungu amuondolee hasad ameen

    ReplyDelete
  6. Umemaliza-kila-kitu-mzee.......HABARI-NDIO-HIYO, watake-ndio-hivyo-wasitake-ndio-hivyo......MWENYE-WIVU-AJINYONGE......au SAGA-CHUPA-UBWIE.....

    ReplyDelete
  7. Umeuwa mzee.....HAPA KAZI TU...watamkubali na watamuelewa tu!!

    ReplyDelete
  8. Does HE Lema have a notion of it???? Forward the message and its link to him and to all hungry faces of so called Upinzani
    It is JPM there never been anybody like him and possibly there will never be
    JPM man of the people

    ReplyDelete
  9. FANYENI KAZI ACHENI UJINGA WA KUSIFIA MJENZI ANAYEJENGA NYUMBA ALIYOBOMOA YEYE MWENYEWE!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Muunge mkono basi hata kama umeona anatengeneza alipochangia kuharibu,na sio kuponda.INAKOLEA?HAPA KAZI TU!

      Delete
    2. KUMUUNGA MKONO MAGUFULI BADO SAAANA!!, "HAPA KAZI TUU!!" USIKURUPUKE NJOO VIJIJINI UONE " HAPA SHIDA TUUU!!, FYUUUUUU!!!

      Delete

Top Post Ad