Elibariki Kingu: Kwa Hili la Makonda, Naomba Niwe wa Kwanza kufukuzwa CCM

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Nilisema Nitanyamaza lakini Nimeshindwa. Nimethibitisha bila mashaka Clouds kuvamiwa na Rc akiwa na ulinzi na askari wenye silaha mpaka kwenye matangazo.

Najua hofu mliyonayo watanzania juu ya huyu Rc.

Ikiwa mamlaka zitaendelea kufumbia macho.Mimi Elibariki Immanuel Kingu mbunge wa CCM nitakuwa wa kwanza kufukuzwa CCM kama kupinga matendo maovu ya Rc huyu itaonekana ni usaliti kwa nchi.

Haiwezekani Rais wetu atukanwe kila kona kwa matendo ya mtu huyu.

Wana CCM ukimya wetu kwenye hili halikubaliki.

Magufuli juzi ametuliza Dodoma kwa kuongea kwa hisia.Idara za usalama kweli mmeamua kuacha tutukanwe?

Naomba sasa niweke kumbukumbu sawa najua mnamchafua kila anayempinga RC huyu kwa matendo yake ambayo yanakiuka utawala bora.

Naomba niwe wa kwanza kufukuzwa CCM kwa kumpinga Rc Makonda

Elibariki Immanuel Kingu
Mbunge.

Source:Jamii Forums
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad