AMWAGIWA Tindikali Kisa Mapenzi...!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MATUKIO yanayohusiana na mapenzi yameendelea kuwa tishio nchini baada ya mwanamke mmoja, Helen John (25) kumwagiwa tindikali na mpenzi wake na kumfanya jicho lake lisione.

Hellen ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kwamhosi kata ya Nkumba wilayani Muheza mkoani Tanga, alipata mkasa huo Aprili 17, mwaka huu.

Akizungumza na Nipashe , alisema chanzo cha tukio hilo ni baada ya kukosana na mpenzi wake huyo na kufanya kuishi tofauti bila mawasiliano hadi siku ya tukio ingawa walikuwa wamezaa mtoto mmoja.

Hellen alisema siku ya tukio kijana huyo aliyemtaja kwa jina la Ally Khamis alikwenda nyumbani kwao kwa lengo la kumbembeleza kurudiana lakini alikataa kwa madai kuwa hataki kuishi na mwanaume huyo kutokana na vitendo vya ukatili ambavyo amekuwa akimfanyia.

Alisema baada ya kukataliwa kijana huo usiku alikwenda kumuwmwagia tindikali machoni na kisha kukimbia lakini ulifanyika msako kwa wanakijiji na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa na kupelekwa katika kituo cha polisi Muheza.

Credit - Nipashe
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad