Kimbunga Nate Chawaua Watu 20 Amerika ya Kati

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kimbunga Nate Chawaua Watu 20 Amerika ya Kati
Kimbunga Nate kimewaua watu zaidi ya 20 nchini Costa Rica, Nicaragua na Honduras huku kikielekea kaskazini upande wa Marekani.
Hali ya dharura imetangazwa katika mataifa kadha ya Amerika ya Kati ambapo watu zaidi ya 20 bado hawajulikani walipo.

Kimbunga hicho kimesababisha mvua kubwa, maporomoko ya ardhi na mafuriko.
Barabara nyingi hazipitiki, madaraja yameporomoka na pia kimesababisha uharibifu mkubwa kwenye nyumba za watu na majengo.
Nchini Costa Rica, watu karibu 400,000 hawana maji na maelfu wengine wameachwa bila makao na wanalala kwenye vyumba vya muda.

Nchini Costa Rica, safari zote za treni zimesitishwa na safari kadha za ndege pia zimefutwa.
Mbuga kadha za taifa ambazo ni maarufu kwa watalii pia zimefungwa kama tahadhari.
Kimbunga hicho pia kimesababisha uharibifu mkubwa kwenye miundo mbinu Nicaragua.
Masachapa Masachapa, about 60km from the city of Managua on October 5, 2017Haki miliki ya pichaAFP

Watabiri wanasema kimbunga Nate kitaimarika na kuwa kimbunga cha ngazi 1 kabla ya kufika tena ardhini pwani ya kusini mwa Marekani siku ya Jumapili.
Kampuni za mafuta zinazohudumu katika Ghuba ya Mexico zimesema zinawahamisha watu kutoka kwenye visima vyake ambavyo vipo maeneo ambayo inatarajiwa kimbunga hicho kitapitia.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad