Baada ya ukimya wa muda mrefu tangu Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu Lissu kushambuliwa kwa risasi nyingi na watu wasiojulikana mchana wa Septemba 8, 2017 mkoani Dodoma, Leo Oktoba 5 Familia ya Mbunge huyo imezungumza na Vyombo vya habari kuhusu Hali ya mbunge huyo kwasasa ambaye anatibiwa Nchini Kenya, imeongea pia kuhusu mwenendo wa Uchunguzi, na kuhusu Dereva wa Lissu.