Kamishina wa Magereza Awapa Ujumbe Mzito Wakina Babu Seya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kamishina wa Magereza Awapa Ujumbe Mzito Wakina Babu Seya
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Juma Malewa amewataka wafungwa waliotolewa kwa msamaha wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli siku ya uhuru, waheshimu mamlaka iliyowatoa na waende wakawe raia wema huko waendako.

Kamishna Malewa amesema anaamini kuwa wafugwa hao walioachiliwa huru kwa msamaha huo wameshajifunza na kujirekebisha na kuwaomba raia wawapokee na kuwatengenezea mazingira ya kuwaingiza katika kazi ili na wao waende sambamba nao.
"Kwa wafungwa waliobaki gerezani wao nao waishi kwa amani, wafanye kazi warekebishike, kwahiyo kwa sasa hata wale wafungwa wa vifungo virefu ambao tulikuwa hatuwatumii huko nyuma kwa kuogopa mambo mbalimbali lakini sasa hivi watakuwa wamejifunza katika hili kwamba ukiishi gerezani ukirekebishika mheshimiwa Rais yupo atatumia mamlaka yake kama alivyopewa na atawasamehe kama alivyowasamehe wengine", amesema Kamishna Malewa.
Kamishna Malewa pia amemuelezea Nguza Viking (Babu Seya )  na kusema kuwa alikuwa mfungwa mwenye nidhamu sana na alipewa cheo kikubwa gerezani yaani Unyampara mwaka mmoja tu alivyoingia gerezani.
9 Desemba mwaka huu siku ya uhuru kwa mujibu ya ibara ya 45 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Rais John Pombe Magufuli alitoa msamaha kwa  wafungwa 61 waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa na wawili Nguza Viking (Babu Seya ) na Johnson Nguza (Papii Kocha ) waliohukumiwa kifungo cha maisha jela.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad