AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na Championi Jumatatu, Meneja wa Mo, Jamal Kisongo amesema kuwa mteja wake huyo anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na Simba baada ya kushindwana na Yanga ambao nao walikuwa wanamtaka huku Msimbazi wao wakitimiza makubaliano waliyokuwa wanataka.
Alisema walifanya mazungumzo na Yanga lakini kuna baadhi ya vitu kwenye mkataba hawakuridhika navyo na walipozu-ngumza na Simba wakakubali kurekebisha baadhi ya vipengele kwenye ule mkataba wa awali hivyo rasmi mteja wake anabaki Simba na leo atasaini kandarasi baada ya ile ya awali kumalizika.
“Kesho (leo) natarajiwa kwenda kusaini mkataba mpya wa miaka mawili na mchezaji Mohammed pale Simba baada ya ule wa awali kumalizika, hivyo tunaongeza mwingine.
“Yanga nao walionyesha kumhitaji lakini kuna vitu walishindwa kukamilisha na tulipozungumza na Simba wamekubali kurekebisha baadhi ya vipengele, hivyo atabaki huko,” alisema Kisongo.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK