Kauli ya Kardinali imeacha maswali mengi kuliko majibu.

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Jana nimebahatika kuisikiliza vyema taarifa fupi (KUNTU) iliyotolewa na mlezi wetu mkuu wa kiroho KARDINALI) ya kuujulisha umma ni nini kilichotokea kupitia chombo chake cha habari TUMAINI. Tunashukuru kwa taarifa yake hiyo ambayo kwa jinsi ilivyotolewa, nina hakika ilifanyiwa kazi ya kina kabla ya kuletwa hadharani.


Kwanza kabisa nashawishika kwa ukurasa wa awali kukubaliana na taarifa yake hiyo kutokana na imani yangu kuu kwake, na inavyojulikana kwa wachache kuwa kada ya UPAPA na UKARDINALI ni kada ambazo wanaozifikia pia wamepitia mambo ya kiintelijensia!


Tunashawishika kuamini hivyo kutokana na jinsi kiongozi huyu wa kiroho ambavyo ameweza kutoa ripoti yake ya kiintrijensia ndani ya chini ya masaa 24! Amesema suala hili lisihusishwe kwa aina yoyote ile na dini au itikadi ya uislamu bali waliofanya kitendo hicho ni WAKRISTO tena wa KANISANI hapo! Na kwa msisitizo akasema kuwa anao uhakika wa kile anachokisema!


Sasa inamaana kwa uweza wa kimungu ambao mtumishi huyu anao na ule wa uintelijensia alionao ameweza kuwasaidia hata polisi wetu kumaliza kazi ya upelelezi katika muda mfupi sana! Sasa kuna haja gani ya kuleta tena CIA? Na kama amesisitiza kuwa taarifa yake aliyoitoa ndiyo ya mwisho, kuna haja gani ya kuwashikilia hao watu wengine, si yeye apelike hiyo ripoti yake polisi ili kazi iwe fupi na amani irejee mioyoni mwa watu na kukata vilimilimi vya watu wengine ambao wanataka kupata umaarufu kupitia SAGA hilo?!


Lakini tukija katika upande wa pili, Je, hatuoni kuwa mtumishi wetu huyu amewahi saaaaaaaaaaaaaaana kutoa ripoti yake hiyo ambayo inaonekana kama hitimisho la SAGA lenyewe?!


Na, Je, kama itatokea ikaja kuapatikina ripoti nyingine tofauti na hii tuliyoaminishwa na mtumishi wa mungu, Je, tutamwamini nani?


Maswali yapo mengi sana kuliko yale ya papo kwa papo ya Waziri mkuu, lakini katika hili nafikiri TAFAKARI ya kina ilitakiwa ichukuliwe kabla ya taarifa hii kutolewa.


TAFAKARI ZAIDI.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

4 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hata wewe hujielewi.. Mara unasema unamwamini pengo.mara hujui wa kumwamini. Kama taarifa ana uhakika nayo akae nayo asubiri ili iweje?? Ukitaka ataje waislamu ama ndo angekuwa hajakosea kuiwasilisha mapema? Kama unamwamini mkuu wa kanisa katoliki nchini hukupaswa hata kuhoji uamuzi wake.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Sawasawa kabisa ndugu huyu admin ndio walewale hana jipya zaidi ya uchochezi

      Delete
  2. Kwa hiyo, ndo nyoka amejing'ata mkia mwenyewe???©ÂºÂªÂªÂªÂªÂªÂªh

    ReplyDelete
  3. Yaan huyu jamaa ndo anasababisha matatizo zaidi ni bora ukatulia kwnz co kuropoka tu




    ReplyDelete

Top Post Ad