Chriss Brown Amwomba Msamaha Karrueche Walipokutana Klabu...Karrueche Amlia Bati na Kumpita Kama Hamjui

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Chriss Akiomba Msamaha huku Karrueche Akiwa Busy na Simu
MAPENZI yanaumiza! Hii ni baada ya staa wa muziki wa RnB, Chris Brown, mwishoni mwa wiki iliyopita kunaswa akiomba kumrudia ex-girlfriend ambaye ni modo na mtangazaji, Karrueche Tran.

Chriss na Karrueche waliachana hivi karibuni kufuatia staa huyo wa Kibao cha Royal kutomjulisha mpenzi wake huyo kuwa ana mtoto aitwaye, Royalty, mwenye umri wa miezi tisa.Karrueche alionekana kuumizwa na tukio hilo na kufikia hatua ya kusema hataki kutumiwa ‘sms’ wala kupigiwa simu na Chris.

Staa huyo alifanya jaribio la kutaka kurudiana na Karrueche usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita, lakini ilishindikana. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kwenye mitandao mbalimbali ya burudani, Chris alianza kumfuatilia ex wake huyo usiku kwenye Klabu ya Playboy huko Chicago ambapo alichukua siti ya VIP iliyo jirani na Karrueche ili iwe rahisi kuonana naye.

Lakini hata hivyo mbinu yake hiyo iligonga mwamba baada ya Karrueche kuamua kuondoka na kushuhudia Chris akimfuatilia kwa nyuma hadi nje ya klabu kabla ya kuonekana akikunja mikono mithili ya mtu anayeomba msamaha mbele ya ex wake huyo.

Mara baada ya Karrueche kuingia kwenye gari yake, Chris alijaribu kutaka kumfuata lakini alizuiwa na marafiki wa modo huyo, ndipo baba Royalty akaamua kulifuata gari lake na kuanza kumfuata kwa nyuma hadi nyumbani.Alipofika akakuta mlango umefungwa ndipo akaanza kupiga kelele sambamba na rafiki zake aliokuwa nao akitaka afunguliwe, hapo tayari ilikuwa usiku mkubwa.

Kuona hivyo Karrueche aliamua kuondoka na kwenda mgahawani ili kuondokana na kero ya kelele lakini Chris alimfuata na huko kabla ya kusikika majibizano baina yao, muda kidogo modo huyo akaonekana akiondoka eneo hilo akiwa peke yake na kuelekea nyumbani kwake.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad