Mastaa Wamliza Kajala usiku, Kisa..!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Imelda mtema
Machozi ya furaha! Staa wa filamu Bongo, Kajala Masanja juzikati alijikuta akiangua kilio baada ya kufanyiwa ‘sapraizi’ na mastaa wenzake katika siku yake ya kuzaliwa.
Tukio hilo lilichukua nafasi usiku wa Julai 22, mwaka huu nyumbani kwake Sinza Afrikasana jijini Dar ambapo akiwa hana hili wala lile, mastaa hao akiwemo Jacob Steven ‘JB’, Jennifer Kyaka ‘Odama’, Zuwena Mohammed ‘Shilole’, Nuh Mziwanda, Leah Richard ‘Lamata’ na wengineo walifika nyumbani hapo mida ya saa 6 usiku kisha wakajibanza nje.

Baada ya muda, Lamata aliyekuwa kwenye msafara huo aligonga mlango wa nyumba ya Kajala na kufunguliwa huku wakiendelea na mazungumzo, Lamata alinyanyuka na kwenda kuzima taa kisha ghafla likaingia kundi la mastaa kila mmoja akiwa ameshika mshumaa unaowaka na keki.
Tukio hilo lilimfanya Kajala apate mshituko na kitendo bila kuchelewa taa iliwashwa kisha mastaa hao wakaanza kumuimbia huku wakimmwagia vimiminika kama vile maji na ‘wine’.
Hali hiyo ilimfanya Kajala alie sana na kuwapa kazi mashosti zake kumtuliza na baadaye walisherehekea hadi asubuhi.

Akizungumzia tukio hilo, Kajala alisema kuwa, furaha aliyokuwa nayo siku hiyo ndiyo iliyomfanya alie kwani amebaini ana watu wengi wanaompenda licha ya kuwepo wachache wenye chuki zao binafsi.
“Kwa kweli sikuamini kile kilichotokea usiku ule ndiyo maana nililia kwa furaha, wenzangu wameonesha upendo wa hali ya juu kwangu,” alisema Kajala huku akifuta machozi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad