AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Habari kutoka kwa shushushu wetu zilidadavua kwamba, mpango mzima ulijiri kwenye bonge la pati ya kuzaliwa kwa Wastara iliyochukua nafasi katika Hoteli ya Sun-Rise iliyopo Kigamboni jijini Dar.
Katika pati hiyo ya kimyakimya, Wastara aliwaalika baadhi ya ndugu na marafiki zake ambapo mtangazaji huyo alikuwa mgeni maalum.
Sosi wetu huyo alitanabaisha kuwa walipofika hotelini hapo, baada ya watu kuanza kupata vinywaji ulifika muda wa keki ambapo Wastara aliwalisha watoto wake na baadhi ya ndugu wa karibu kisha alimuita mtangazaji huyo na kulishana naye keki kwa staili hiyo iliyogeuka gumzo.
“Unajua wale ni wapenzi lakini siku zote hawajawahi kuweka wazi uhusiano wao hadharani lakini sasa naona Wastara ameamua kuweka kila kitu wazi,” kilisema chanzo hicho.
Baada ya kumegewa ‘ubuyu’ huo, Ijumaa Wikienda lilizungumza na Wastara ambapo alifunguka kuwa wageni wote aliowaalika aliwalisha keki kwa staili hiyo kuonesha ni wapenzi wake wa kweli.
“Jamani wageni wangu wote niliowaalika niliwalisha kwa staili hiyo na hao ndiyo wapenzi wangu wa ukweli kwa sababu hata watoto wangu na dada zangu niliwalisha kwa mdomo pia,” alisema Wastara.
Chanzo: GPL
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Eda ilisha isha tatizo nini sasa
ReplyDelete