Kampuni ya UDA Yaibuka na Kusema Haya Kuhusu Familia ya Kikwete Kumiliki Kampuni Hiyo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group, Robert Kisena ameeleza kusikitishwa na taarifa zisizo za kweli zinazoihusisha familia ya Rais mstaafu, Jakaya Kikwete na umiliki wa Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda) na kusisitiza kuwa yeye ndiye mmiliki halali.

Kisena alidai kwa muda mrefu watu wenye nia mbaya dhidi yake, wamekuwa wakihoji umiliki wa shirika hilo licha ya kuonyesha vielelezo vyote. Alisema taarifa zilizosambaa hivi karibuni zinazodai kuwa anaimiliki Uda kwa ushirikiano na Khalfan ambaye ni mtoto wa Kikwete hazina ukweli.

Alidai kuwa Kampuni ya Simon Group ambayo ilisajiliwa Mwanza 2007, inamilikiwa na watu wanane wa familia ya Kisena isipokuwa Profesa Juma Kapuya ambaye ana asilimia tano ya hisa kwenye kampuni hiyo.

“Kampuni hii inamilikiwa na watu wanane, hata mkisoma hizi nyaraka mtaona majina ya watu hao ambao ni mimi, wanangu; Simon, Gloria, Kulwa na George; mdogo wangu William Kisena, mama yangu Modesta Pole na Profesa Kapuya.

“Hakuna jina la Khalfan Kikwete hapa, sijui hizo taarifa watu wanazitoa wapi,” alihoji Kisena huku akionyesha vielelezo.

Alisema hata wakati kampuni hiyo inaanzishwa, Khalfan alikuwa mtoto mdogo ambaye asingeweza kumiliki kampuni hiyo ambayo inakua kwa kasi.

Kisena alidai taarifa hizo za uongo zinaenezwa na watu ambao ni washindani wake kibiashara na wengine ni maadui wa kisiasa wa Kikwete.

Alisema yeye ni kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na amekuwa hivyo siku zote, lakini hajihusishi na siasa bali anafanya biashara.

“Kama kuna wanaoichafua familia ya Kikwete waache kuniunganisha na mimi, sifanyi siasa.

"Na kama kuna wanaonichafua kibiashara basi waache kuiingiza familia ya Kikwete, wapambane na mimi kwenye biashara,” alisema Kisena.

Hata hivyo, mwenyekiti huyo alisema kampuni yake ya Uda RT ndiyo itakayoendesha mradi wa mabasi yaendayo kasi na kuwa nauli zilizopendekezwa zilitokana na tathmini ya gharama halisi za uendeshaji wa mradi huo.

Alisema baadhi ya vitu vilivyowafanya wapendekeze nauli hizo kuanzia Sh700 mpaka Sh1,200 ni pamoja na kulipia barabara za Dart.

Pia, alisema mabasi hayo yatakuwa hayakai vituoni kwa hiyo huenda wakati mwingine yatakuwa yanatembea bila abiria.

“Sababu hizo ndiyo zimetufanya tupendekeze nauli hizo, lakini tuko kwenye mazungumzo na Serikali ili waondoe malipo ya barabara ili nauli ipungue.Mazungumzo yanaenda vizuri, ninaamini nauli zitapungua,” alisema.

Kisena alisema ifikapo Machi, mwaka huu, Kampuni ya Uda itaorodheshwa kwenye Soko la Hisa ili wananchi waweze kumiliki wenyewe kampuni hiyo.

Alisema wanaendelea kufanya mipango kwa ajili ya kuuza asilimia 70 ya hisa kwa wananchi wote.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad