Mtuhumiwa Anayesakwa na Polisi Awatumia Polisi Selfie ya Picha yake na Kusema Waliyotumia ni Mbaya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwanamume anayesakwa kwa makosa la kuteketeza na kuharibu mali ametuma picha ya selfie kwa maafisa wa polisi akisema picha iliyotumiwa na maafisa hao katika tangazo la kutafutwa kwake haikuwa ya kupendeza.

Donald "Chip" Pugh aliwatumia maafisa wa polisi picha aliyojipiga mwenyewe na kuandika ujumbe unaosema: "Hii hapa picha yangu nzuri, hiyo mliyotumia ni mbaya sana”.
Polise katika mji wa Lima, jimbo la Ohio, walikuwa wamepakia picha kwenye ukurasa wao wa Facebook wakiomba msaada wa kumtafuta Bw Pugh.
"Picha hii ilitumwa na Bw Pugh mwenyewe," kituo cha polisi cha Lima kiliandika kwenye ukurasa wa Facebook.

"Tunamshukuru kwa msaada wake lakini sasa tungeshukuru hata zaidi kama angejitokeza na kuzungumza nasi katika kituo cha polisi kuhusiana na mashtaka yanayomkabili. "
Polisi walisema anatafutwa kwa mashtaka kadhaa na amri ya kukamatwa kwake inahusiana na kushindwa kufika kituo cha polisi kama ilivyoagizwa.

"Bwana, walinikosea," Bw Pugh aliambia kituo cha Redio cha Ohio, akieleza ni kwa nini akawatumia polisi picha hiyo ya selfie.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad