Besigye Apinga Matokeo ya Urais Uganda...Waangalizi Wasema Uchaguzi Ulikuwa Katika Mazingira ya Hofu na Kudhalilishwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mmoja wa wapinzani wakuu katika uchaguzi mkuu uliofanyika Alhamis wiki hii nchini Uganda, Dkt Kizza Besigye, amepinga matokeo ya uchaguzi huo.

Dkt. Besigye ambaye amekuwa akizuiliwa nyumbani kwake tangu siku ya Ijumaa amesema kuwa raia nchini Uganda wameshuhudia udanganyifu mkubwa katika uchaguzi huo, ambao haujahi kufanyika katika taifa hilo.

Kanali huyo mstaafu ameuelezea uchaguzi huo kuwa si halali na kuwa ni sawa na mapinduzi ya kijeshi.
Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa jana, Rais wa muda mrefu wa taifa hilo Yoweri Kaguta Museveni, alitangazwa mshindi.

Rais Museveni ambaye amekuwa mamlakani kwa miaka thelathini sasa, alipata zaidi ya asilimia 61 ya kura huku Besigye akijipatia asilimia 35 ya kura.

Waangalizi wa kimataifa wamesema kuwa uchaguzi huo uliandaliwa katika mazingara ya hofu na kudhalalishwa.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad