AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wapiganaji wa Kundi la Boko Haram wamewateka nyara wanawake 16 katika eneo la mashambani, Kaskazini Mashariki mwa Jimbo la Adamawa.
Vyanzo vya habari vilisema wanawake hao walitekwa msituni, walipokuwa wakitafuta kuni na wengine walikuwa wakivua samaki kando ya mto.
Wanawake hao hadi sasa hawafahamiki mahali walipohifadhiwa na watekaji.
Kundi hilo lililoenea nchini humo, limekuwa likijihusisha na vitendo vya utekaji wa mara kwa mara. Awali, liliwateka wasichana ambao ni wanafunzi zaidi ya 200 ambao mpaka sasa hawajapatikana.
Wakati huohuo, Jeshi la Nigeria limewakomboa zaidi ya watu 800, waliokuwa wakishikiliwa na kundi hilo katika vijiji kadhaa, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Mateka wengine walikombolewa katika Jimbo la Borno, huku 520 wakikombolewa katika Kijiji cha Kisuma, baada ya mapambano kati ya wanajeshi hao na wapiganaji wa kundi hilo, mateka wengine 309 waliokolewa katika vijiji vingine 11 vinavyodhibitiwa na kundi hilo.
Rais wa nchi hiyo, Muhammadu Buhari alipokuwa anaingia madarakani alisema atahakikisha anapambana na kundi hilo
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK