Jide: Ray C Anahitaji Marafiki Sahihi Katika Kipindi Hichi Kigumu..la Sivyo....

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ a.k.a Jide, amesema msanii mwenzake, Rehema Chalamila, anahitaji marafiki sahihi ambao watamsaidia katika kipindi hiki kigumu.

Ray C ambaye amewahi kujihusisha na madawa ya kulevya, kwa sasa ameripotiwa kurejea kwenye matumizi hayo huku mara kadhaa ikiripotiwa kuwa mrembo huyo aliyekimbiza na Kibao cha Na Wewe Milele, amerejea kwenye utumwa huo wa madawa hayo ambayo ni hatari.

Jide alizungumza hayo Ijumaa iliyopita alipokuwa akizindua kichupa chake cha Ndi Ndi Ndi kwenye Kipindi cha Friday Night Live kinachorushwa na East Africa Television na Radio. Alisema alikuwa hajakutana muda mrefu na Ray C kabla ya juzikati alipokwenda kumsalimia nyumbani kwake.

“Ray C alikuja kunisalimia nyumbani, tulizungumza kwa kuwa hatukuwa tumeonana kwa muda mrefu sana, kipindi anachopitia sasa ni kigumu, ni mtu ambaye anahitaji watu wa kuwa naye karibu na marafiki sahihi lakini siwezi kusema kama nilisema namsaidia au chochote.

“Lakini wapo watu ambao aliniambia tayari wapo kwenye mchakato wa kumsaidia, kwa hivyo tunawapa nafasi watu ambao wanaweza kutoa msaada zaidi,” alisema Jide.

Chanzo;GPL
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad