Petit Money Aelezea Uhusiano Wake Ulivyo Sasa na Shemeji yake Diamond na Bosi wake Wema Sepetu (Video)

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ahmed Hashim Ngahemela kama anavyojulikana zaidi kwa jina la Petit Money anafahamika zaidi kwa kuwa mmoja wa waliokuwa wafanyakazi wa Wema Sepetu na pia aliyekuwa mume wa dada yake na Diamond, Esma.


Tumezungumza naye kutaka kufahamu uhusiano wake na shemeji yake Diamond ukoje licha ya kuwa upande wa Wema ambaye haziivi tena na Diamond.

“Mitihani inakuwa mingi, ni lazima itokee lakini watoto wa kiume mitihani tumeumbiwa sisi. Mitihani mingi sana imetokea, wakati mgumu sana umetokea baina ya timu zile mbili kuwa tofauti na mimi ndio nimebase sehemu zote, huku na huku lakini nashukuru niliplay part yangu vizuri,” amesema Petit.

“Mimi sina tatizo na Diamond, ni shemeji yangu na ni family sababu mimi nilishazaa na dada yake hata kama ikawaje siwezi nikawa na tatizo naye, tukikutana njiani tunasalimiana, mimi ninadili ntampigia, hatuna tatizo.”

Kwa sasa Petit ni meneja wa Billnass na Nuh Mziwanda, kitu ambacho anasema kimesababisha maelewano hafifu na bosi wake wa zamani, Wema Sepetu.

“Mimi sidhani kama nina tatizo na Wema. Ndiye aliyenifanya mimi nijulikane na Wema ndiye mtu ambaye mimi nimetoka naye mbali sana miaka tisa. Kwahiyo hata kama nikiwa nimegombana naye siwezi nikasema siongei naye, kwahiyo mimi nahesabia sina tatizo naye kama watu wanavyodhani,” ameongeza.

Tazama zaidi interview hapo juu.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad