Hata Kuziba Midomo ni Demokrasia-Rais Magufuli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Akizungumza leo Ikulu Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amewataka wanasiasa waliopewa nafasi za uwakilishi na wananchi wajikite zaidi katika kuwahudumia ili kuwaletea maendeleo waliyowaahidi wakati wa kampeni.

Rais Magufuli amesema kuwa wakati wa uchaguzi umekwisha hivyo wakati wa siasa sasa nao umekwisha hivyo amewataka viongozi wao wa siasa kushirikiana nae katika kuleta maendeleo ikiwemo kumpa ushauri ambao nae ataufanyia kazi kwa maendeleo ya Wananchi wote.

Dkt. Magufuli amesema kuwa kamwe hatomvumilia mtu yoyote ambae atamchelewesha katika harakati zake za kuwaletea maendeleo wananchi, hivyo ni vyema wakaungana kwa pamoja katika kufanikisha suala hilo.

Rais Magufuli amesema wabunge waliochaguliwa waelekeze nguvu katika kuwasemea wananchi kwa kufuata demokrasia ingawa hata kuziba midomo ni demokrasia ya aina yake lakini amevitaka vyama vyote kushirikiana nae katika kulileta taifa maendeleo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

13 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Sawa kabisa Mkuu... Siasa siku zote zinapewa uwanja wakati wa kumwaga sera.. Ili wananchi wapime na watafakari halafu wamchague kiongozi ambaye wamekubaliana na sera zake. Pindi matokeo yameshatangazwa na chama tawala kimeshika uongozi.. Siasa zote sinasitishwa na vyama vyote vinakuwa na mewlekeo mmoja wa kujenga nchi imara na Maendeleo.. sababu ni kwamba nchi ni ya wananchi na wanaoguswa na adha za maisha hazichaguwi huyu wa chama hiki au kile .. ni wote sawa.. Alichoomba Mkuu ni sisi sote kuwa wazalendo na kushirikia nae katika ujenzi wa taifa letu na Tuelete Maendeleo kwa michango yetu sisi sote na siyo kujibagua kuwa mimi ni chuki na sikubaliani na serikali hivyo ni kwamba utajiweka nyuma na Hii treni ya maendeleo itakupita na ukija tahamaki utajikuta uko peke yako.. Kwa hiyo kaeni mkikumbuka wajibu wa kuchangia Maendeleo ni wakwetu wote na kushiriki katika michango yenu ni wajibu wetu sisi wote bila kijali wewe uko kaskazi wala kusini... Tuwe Wazalendo wenye Nia na Lengo la kuleta Maendeleo kwa Ajili ya Watoto wetu na Vizazi vyetu.. Sisi tutakuwa ni watu wakusimuliwa lakini Kazi tuifanye sasa... Nakuombeni kaeni tafakarini halafu mpate jibu.. Leo tunae JPJM ameamua na anafanya ambayo ingekuwa ni mwingine ingechukua miaka zaidi ya Hamsini.. Huyu amekataa Ubadhirifu / Ufisadi na amepiga vita Corruption in all its forms na Amerudisha Nidhamu ambayo ilikuwa imepotea mpaka watu wakaweza kujiwekea mazingira ya Hewa kila upande.. Yeye anayakemea na anayakomesha. Leo ukiingia Ofisini kwa mtumishi wa umma anakusikiliza na anakuhudumia ipasavyo.. Je enzi zile utamkuata? na ukimkuta atakuletea mlolongo wa sababu kuonesha ukitakacho ni impossile.. na ukimpa Hongo unakipata.. leo haya yote yamefifia na karibu kila siku zinavyokwenda yanakufa... Wapi tungeweza kuota wacha kufikiria kwamba haya yangeondoka Tanzania yetu. Na sasa yanatoweka.. Nakuombeni wote tujiunge na tuweze kushirikiana na Mtukufu Rais JPJM ili tumrahisishie malengo yake ya kutusaidia sisi wananchi ... Siasa ni wakati wa kampeni. Serikali imepatikana siasa zote zinasitishwa hii ni Duniani kote.. Uelewa wetu ni bado kwa ajili tulilelewa na Awamu ambazo hazikuzingatia na bado tulikuwa ni wageni na jambo hili. Sasa tunasema Hapa ni Kazi tu. ushirikiano wenu na Busara zenu na michango yetu yenye manufaa na yasiyo na chuki wala Tamma katika mioyo yenu. Tutayapokea na Mazuri baada ya kuyapima Tutayashughulikia na kuyaleta katika Mifumo ya Maendeleo ya Nchi na Wananchi... Mungu Ibariki Tanzania yetu ya Amani Usalama Na Upendo..

    ReplyDelete
  2. Sawa kabisa Mkuu... Siasa siku zote zinapewa uwanja wakati wa kumwaga sera.. Ili wananchi wapime na watafakari halafu wamchague kiongozi ambaye wamekubaliana na sera zake. Pindi matokeo yameshatangazwa na chama tawala kimeshika uongozi.. Siasa zote sinasitishwa na vyama vyote vinakuwa na mewlekeo mmoja wa kujenga nchi imara na Maendeleo.. sababu ni kwamba nchi ni ya wananchi na wanaoguswa na adha za maisha hazichaguwi huyu wa chama hiki au kile .. ni wote sawa.. Alichoomba Mkuu ni sisi sote kuwa wazalendo na kushirikia nae katika ujenzi wa taifa letu na Tuelete Maendeleo kwa michango yetu sisi sote na siyo kujibagua kuwa mimi ni chuki na sikubaliani na serikali hivyo ni kwamba utajiweka nyuma na Hii treni ya maendeleo itakupita na ukija tahamaki utajikuta uko peke yako.. Kwa hiyo kaeni mkikumbuka wajibu wa kuchangia Maendeleo ni wakwetu wote na kushiriki katika michango yenu ni wajibu wetu sisi wote bila kijali wewe uko kaskazi wala kusini... Tuwe Wazalendo wenye Nia na Lengo la kuleta Maendeleo kwa Ajili ya Watoto wetu na Vizazi vyetu.. Sisi tutakuwa ni watu wakusimuliwa lakini Kazi tuifanye sasa... Nakuombeni kaeni tafakarini halafu mpate jibu.. Leo tunae JPJM ameamua na anafanya ambayo ingekuwa ni mwingine ingechukua miaka zaidi ya Hamsini.. Huyu amekataa Ubadhirifu / Ufisadi na amepiga vita Corruption in all its forms na Amerudisha Nidhamu ambayo ilikuwa imepotea mpaka watu wakaweza kujiwekea mazingira ya Hewa kila upande.. Yeye anayakemea na anayakomesha. Leo ukiingia Ofisini kwa mtumishi wa umma anakusikiliza na anakuhudumia ipasavyo.. Je enzi zile utamkuata? na ukimkuta atakuletea mlolongo wa sababu kuonesha ukitakacho ni impossile.. na ukimpa Hongo unakipata.. leo haya yote yamefifia na karibu kila siku zinavyokwenda yanakufa... Wapi tungeweza kuota wacha kufikiria kwamba haya yangeondoka Tanzania yetu. Na sasa yanatoweka.. Nakuombeni wote tujiunge na tuweze kushirikiana na Mtukufu Rais JPJM ili tumrahisishie malengo yake ya kutusaidia sisi wananchi ... Siasa ni wakati wa kampeni. Serikali imepatikana siasa zote zinasitishwa hii ni Duniani kote.. Uelewa wetu ni bado kwa ajili tulilelewa na Awamu ambazo hazikuzingatia na bado tulikuwa ni wageni na jambo hili. Sasa tunasema Hapa ni Kazi tu. ushirikiano wenu na Busara zenu na michango yetu yenye manufaa na yasiyo na chuki wala Tamma katika mioyo yenu. Tutayapokea na Mazuri baada ya kuyapima Tutayashughulikia na kuyaleta katika Mifumo ya Maendeleo ya Nchi na Wananchi... Mungu Ibariki Tanzania yetu ya Amani Usalama Na Upendo..

    ReplyDelete
    Replies
    1. Utatoaje huo mchango wakati kila kitu kimebinywa, utaongea wakati hujui kinachoendelea bungeni!! wawakilishi wetu hawaruhusiwi kuongea na nyinyi kwenye mikutano ya hadhara, bungeni wakitoa hoja zinazimwa (wanafungiwa)!! utatoa ushauri gani wakati unaishi gizani!? taa inawashwa ili iwekwe juu ya meza na siyo chini ya meza!!! wabunge tumewaweka ili tuwasikie siyo wakalale bungeni na sisi tusijue chochote kinachoendelea!! hiyo siyo haki hata kidogo... Wote tumemkubali rais wetu, ila inaoneka majipu yamerudi upinzani na hao wa ccm wamekuwa ni watakatifu badala ya majipu!!! this is not fair at all!!!

      Delete
  3. But this your thinking mr president
    Usilazimishe watu wafuate yako
    Do it as president
    Wabunge na madiwani they have their own vision according wapi wanatoka
    By the mr president watanzania wanakusapport na kazi yako
    Pls ruhusu uhuru wa habari
    Wasaizidi wanakudandanya kwa hili
    Uhuru wa habari Kama utasoma wewe
    Mkewe au watoto au watu karibu watakuambia makosa yako
    Nobody is perfect

    ReplyDelete
    Replies
    1. Wewe ndio kichuguu kisichokuwa na uelewa na dunia ni wale msafara wa mamba watu wasiokuwa na shukurani eti wabunge na madiwani they have their own vision ina maana nawao ni maraisi wahukumu kama alivyo raisi hata bata atakuwa anayo vision yake kweli tunataka maendeleo yatoke mbinguni

      Delete
  4. anonymous 7:45 huna akili acha ujinga mwache rais afanye kazi yake huu ni wakati wa kazi sio siasa hususani tulicheleweshwa muda mrefu mkombozi kaja mwache afanye kazi wapinzani kazi yao ni kupinga tuu HAPA KAZI TU. KILAZA NINI MWANANGU

    ReplyDelete
  5. dikteta siku zote ana ona yuko sawa na siku zote hapendi kukoselewa,anapenda kuambiwa ndiyo mzee.Kwani yeye mungu?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Tutolee sie huko!!! Hao waliopita ndio walikuwa madikteta kwa kujipendelea wenyewe na makundi yao na familia zao. Kutwa kutuibia, tumechoka kuibiwa na kuendelea kutabika tu kwa umasikini. Na hizo mali asilia ni cake nazo tule wote. Na kodi zetu tuone kila kitu kinafanyika. Sio kutunisha mifuko yao tu. Hapa Baba Magufuri tupeleke kwenye karne ya millenium uwanja ni wako wewe kocha sisi wachezaji ,atakaeharibu tu mtupe nje kule kwa kadi nyekundu Mpka kila mtu akue hili Taifa kila mtu ana haki ya kuthaminiwa na kueshimiwa tena kwa herufi kubwa tunapenda kusema NDIO MZEE. WEWE NDIYO UTAILETEA HESHIMA TAIFA LETU LILILO LALA USINGIZI WA MUDA MREFU.

      Delete
    2. acha upumbavu wako kwa nini umlinganishe Rais wetu na Mungu? fala sana wewe, mwache afanye kazi yake wewe kaa kubwabwaja tu.

      Delete
  6. mheshimiwa uku usije sijawahi kusikia wanakusema vizuri mitaa ya huku kwetu nahisi hawakupendagi!

    ReplyDelete
  7. siasa ni kazi,hawa wanasiasa tunaowaona wanazunguka kila siku, hiyo ndio kazi yao. vyama pinzani moja ya kazi yake ni kuangalia mapungufu yaliyopo kwenye serikali iliyopo madarakani na kushauri dawa ya mapungufu hayo. nchi imetoka mbali kufika hapa tulipo katika nyanja nyingi hasa swala la demokrasia. tunajua hulka ya binadamu hatupendi kukosolewa. lakini maendeleo mazuri yanataka kuwepo kukosolewa ili tuweze kujirekebisha. Tuliombee Taifa letu amani umoja na kuelewana ili tufike tunapokwenda,kwani safari ni ndefu. Mungu ibariki Tanzania.

    ReplyDelete
  8. Wote mnaoita utawala wa sasa ni wa udikteta mlikua mnafaidika na ufisadi mmebnwa mbavu sasa mnaona watu madekteta na bado hama nchi kama hutaki kukaa Tanzania sasa watu adabu hakuna pesa zaa kuja kwenye ndoooo

    ReplyDelete

Top Post Ad