Ripoti ya Jeshi la Polisi Dar es Salaam Baada ya Kumalizika kwa zoezi la uhakiki wa silaha, Pia Wamezungumzia Kiasi Walichokusanya Ndani ya Siku 6

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Jeshi la Polis kanda Maalumu jijini Dar es salaam limekamata watuhumiwa sugu 1,065 kwa makosa mbalimbali yakiwemo unyang’anyi wa kutumia nguvu, wizi wa maungoni, wapiga debe, wavuta bangi, kikosi cha mbwa mwitu, watuhumiwa hao wamekamatwa kwa nyakati tofauti tofauti katika maeneo mbalimbali jijini Dar es salaam.

Hayo yamesemwa na kamishina wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaam Simon Sirro alipokua akiongea na waandishi wa habari mapema hii leo, Sirro alisema kuwa kukamatwa kwa watuhumiwa hao kumekuja baada ya kufanya operesheni kali katika maeneo mbalimbali jijini humo.

Aidha pamoja na kufanikisha zoezi hilo kwa watuhumiwa hao,jeshi hilo pia wamekamata lita 952 za pombe aina ya gongo,bangi puli 227, kete 210, na misokoto144 kutoka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.

Katika hatua nyingine ,kikosi cha kupambana  na wizi wa simu cha polisi kimefanikiwa kuwatia hatiani watuhumiwa watatu(3) kwa makosa ya uporaji wa simu katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa kinondoni,watuhumiwa hao ni Richard Augustino (18), Abdallah Chande (36),Abdallah Said (22) wote wakazi wa jijini  Dar es salaam.

Hata hivyo kamanda Sirro aligusia  zoezi zima la uhakiki wa silaha na kusema kuwa lilienda vizuri na watu walijitokeza kwa wingi japo kuna changamoto kadhaa zilizojitokeza

Kamanda  Sirro amesema  idadi ya watu waliojitokeza kuhakiki silaha kwa wilaya zote tatu ni 11,602 na jumla ya silaha 14107 zilihakikiwa.

Pia kasema Jumla ya silaha 66 zilisalimishwa kutokana sababu mbalimbali ikiwamo mmiliki wa silaha kuwa na umri mkubwa na kushindwa kumudu silaha. Zoezi la uhakiki wa silaha limeiingizia Serikali mapato kiasi cha Mil 198.8

Jeshi hilo kupitia kikosi cha usalama barabarani kanda maalumu ya Dar es salaam limeweza kujikusanyia kiasi  cha shilingi 562,860,000/= kutokana na ukamataji wa makossa mbalimbali ya usalama barabarani kuanzia tar 15/7/2016 hadi 21/7/2016.
   Idadi Ya Pikipiki Zilizokamatwa  -1,413
     Idadi Ya Magari Yaliyokamatwa  –17,349
     Daladala Zilizokamatwa           -7220
     Magari Mengine (Binafsi Na Malori)- 10,129
     Jumla Ya Makosa Yaliyokamtw-  18,762
6. Bodaboda Waliofikishwa Mahakamani Kwa Makosa Ya Kutovaa Helmet Na Kupakia Mishkaki   ni 49
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad