Waziri Kigwangalla: Kuanzia Sasa Lazima Kila Mwananchi Awe na Bima ya Afya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Naibu Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Dkt. Khamis Kigwangala amesisitiza kuwa kuanzia sasa itakuwa ni lazima kwa kila Mtanzania kuwa na Bima ya afya,huku akiwatoa hofu wananchi wasio na uwezo kwamba serikali kupitia Sera ya taifa ya afya ya mwaka 2007, itakuwa tayari kugharamia matibabu ya makundi maalumu ya kijamii wakiwemo wazee wenye umri wa zaidi ya miaka 60, watoto chini ya umri wa miaka mitano na watu wenye magonjwa ya kudumu.

Naibu Waziri kigwangala, ameyasema hayo wakati akifunga Maadhimisho ya miaka 50 ya utume wa injili kwa waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato Kirumba Mwanza yaliyofanyikia katika uwanja wa CCM Kirumba, yakiwa yametanguliwa na zoezi la utoaji wa huduma za afya bure kwa wakazi hilo zilizofanywa na madaktari bingwa wa macho,meno,kibofu cha mkojo,tezi dume,kisukari na saratani ya shingo ya kizazi kwa siku saba mfululizo.

Sherehe za miaka 50 tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo la Waadventista wa Sabato katika jiji la Mwanza mnamo mwaka 1935,lililopo chini ya jimbo la Nyanza Kusini,ambalo hadi sasa limefikisha makanisa 84 pia zimehudhuriwa na Naibu Waziri wa ardhi, nyumba na makazi Mh.Angelina Mabula, ambaye amesema kazi kubwa ya kanisa ni kuendelea kuokoa maisha ya waumini wake kiafya na kiroho pamoja na kusimamia maadili mema ndani ya jamii.

Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wasabato tanzania Dk.Godwin Lekundayo, ameiomba serikali kuharakisha usajili wa hospitali ya Pasiansi inayojengwa na kanisa hilo ili iweze kuanza kutoa huduma kwa muda uliopangwa, lengo la kanisa la SDA jimbo la Nyanza Kusini ni kuifanya hospitali hiyo kutoa huduma za matibabu ya rufaa ili kuokoa maisha ya watu.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad