Watumia Jina la Tibaijuka Kutapeli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MBUNGE wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka amehadharisha umma dhidi ya ukurasa uliotengenezwa katika mtandao wa kijamii wa Facebook ukitumia jina lake, kuwa anakaribisha maombi ya watu wa kuajiriwa kwenye shirika linalosaidia watu kuondokana na umasikini.

Profesa Tibaijuka ambaye amesisitiza kuwa ukurasa huo si wake, ametaka taarifa zilizomo zipuuzwe akisema umetengenezwa na matapeli wanaochafua jina lake ambao wanadai watu watakaopitishwa, watapata fursa ya kufanya kazi katika nchi mbalimbali Afrika.

“Ukurasa huu sio wa kwangu wala siufahamu. Hivyo basi na taarifa zote zilizoandikwa kwenye ukurasa huu ni uongo na hazitoki kwangu…nawaomba mpuuze taarifa hizi na wala msitume taarifa zenu kupitia parua pepe kama inavyoelekeza,” Profesa Tibaijuka aliliambia gazeti hili jana.

Taarifa zilizopo kwenye ukurasa huo, zinakaribisha watu kutuma maombi ya kufanya kazi na shirika lisilo la kiserikali (NGO) linaloshughulika na kupunguza umasikini uliokithiri katika Afrika.

Wenye uhitaji wanatakiwa kutuma taarifa kwenye barua pepe iliyoonesha jina la Profesa Tibaijuka huku ikielezwa kuwa sifa zinazotakiwa ni kuanzia elimu ya sekondari na kwamba wanaohitaji wawe tayari kufanya kazi katika nchi nyingine za Afrika.

Aidha, taarifa hizo zinasisitiza kuwa wanachama wa skauti na klabu ya Lions watapewa kipaumbele. Mbunge huyu aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Makazi Duniani (UN-Habitat), alisema taarifa juu ya utapeli huo zimekwishavifikia vyombo vya usalama na wanaendelea na uchunguzi kubaini na kuwakamata mara moja wahusika.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. opps watumie jina lako wewe anna nani duniani hata tanzania hata watu wa jimbo wengine hawakujui
    akanana kaliwa koko

    ReplyDelete

Top Post Ad