AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Aunty aliyekuwa kwenye kipindi cha FNL cha EATV amesema movie ambayo amekuja nayo sasa ni ya viwango vya hali ya juu, na ina utofauti na movie zote alizowahi kucheza siku za nyuma kwa kuachana na mambo ambayo anadai kuwa hayakuwa na maana kwenye movie.
Movie hiyo inayokwenda kwa jina la 'Christmas Eve' ambamo Aunty anatumia jina la Salome, inazinduliwa leo na itakuwa LIVE kupitia EATV kuanzia saa 3:00 usiku, ambapo Aunty pia ameeleza sababu za kuifanyia uzinduzi movie hiyo kuwa ni pamoja na kuwaonesha mashabiki wake utofauti wa movie hiyo na kazi zake zamani
"Tumefanya kitu tofauti, siyo kama ile ya zamani ya kwenye makochi, unaingia shikamoo baba, halafu mambo yanakuwa yaleyale, tumeona tuzindue kwa kishindo ili kuwaonesha watu utofauti" Amesema Aunty.
Katika hatua nyingine Aunty alikiri kuwa yeye ni mjamzito na kwamba hicho ni kitu ambacho hawezi kuficha wala hana sababu ya kufanya hivyo kwa kuwa ujauzito haufichiki na pia kuweka wazi kuwa sasa amebadili mtindo wake wa maisha na kuachana na mambo aliyoyaita kuwa ni ya kitoto.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK