MZIKI ya Darassa ilivyogeuka Wimbo wa Taifa Ndani ya Wiki Moja

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Hii hutokea kwa nadra sana na tena kwa wasanii wachache tu wenye ngekewa zao. Kama ni soka, basi Darassa amepiga hat-trick. Kama Utanipenda, Too Much na Muziki ni nyimbo zilizobadilisha upepo katika maisha ya muziki ya Darassa.

Kama Utanipenda na Too Much zilikuwa ni kama mvua za rasha rasha zilizoashiria kuwa kuna mvua kubwa inataka kunyesha. Bila promo kubwa, Novemba 23, Darassa aliachia wimbo wake Muziki ambao ungekuja kuwa gia ya mwisho wa kuashiria kuwa gari limeondoka rasmi.

Hii hutokea kwa nadra sana na tena kwa wasanii wachache tu wenye ngekewa zao. Kama ni soka, basi Darassa amepiga hat-trick. Kama Utanipenda, Too Much na Muziki ni nyimbo zilizobadilisha upepo katika maisha ya muziki ya Darassa.

Kama Utanipenda na Too Much zilikuwa ni kama mvua za rasha rasha zilizoashiria kuwa kuna mvua kubwa inataka kunyesha. Bila promo kubwa, Novemba 23, Darassa aliachia wimbo wake Muziki ambao ungekuja kuwa gia ya mwisho wa kuashiria kuwa gari limeondoka rasmi.

Naye mrembo mwingine, Elizabeth ‘Lulu’ Michael amepost video akifurahia wimbo huo na kuandika: Mama Micah on the One n Two…Shikamoo @laviemakeup Sio Simba,Sio Chui,Sio Mamba….Kazi Yangu Tu inatosha kujigamba 💃Nasikia huu ni Wimbo wa Taifa😝.”

“Mimi Wakazi nasema hivi, Ndio Kwa sasa DARASSA is one of the hottest rap artist in the country, period. (Nilikuwa Dodoma na Wimbo wake mpya unafanya vizuri kuliko hata wa Wasafi mpya,” aliandika Wakazi.

Naye producer Jors Bless ameandika: Jamaa ameula bana……. I’m happy he found a style na sound ya kumtambulisha, you listen to nyimbo za Darassa from ile alofanya na Blue I think Heya haye or whatever it’s like from there aliamza kutembea na template ya muziki wake, he found himself….. That’s what wasanii wengi wanafeli, hawajijui wanafit wapi, at the end of the day they want to do everything hence a confusion because there is no identity, darassa found his.”

Ndani ya wiki na nusu, video ya wimbo huu imeshavutia views zaidi ya 788,000 – kitu ambacho ni nadra kwa msanii anayefanya Rap. Umma umeukubali wimbo huu na ni kweli kuwa kile alichokisema katika miongoni mwa nyimbo zake za mwanzo kabisa, ‘Sikati Tamaa’ kimemsaidia kufika hapo alipo leo.

Naamini kuwa Darassa anaelekea kuanza kuifaidi fedha ya muziki ambayo ni wasanii wachache wapo kwenye nafasi hiyo. Kwakuwa kama alivyosema Jors Bless kuwa ametambua sound yake, rapper huyu ataendelea kukwea ngazi na kama ataendelea kutengeneza hits zaidi, Tanzania inaenda kupata msanii mwingine wa rap mwenye ushawishi mkubwa siku za usoni.

Nauona muziki ukitumika kwenye kampeni na matangazo ya biashara ya matangazo makubwa. Kwa jinsi wimbo wake unavyofanya vizuri, rapper huyu hakwepeki kwenye kila tamasha kubwa. Shabiki mmoja anadai kuwa muitikio wa kushangaza wa wimbo wake, unadhihirisha kuwa woga uliopo kuwa timu zinadidimiza muziki wa Tanzania hauna maana. Anaamini kuwa kila msanii atakayeweza kufanya muziki mzuri ana nafasi ya kumega mkate wa tasnia hiyo.

Fredrick Bundala
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad