AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Notisi iliyotolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma – PSPF ambao ndio wamiliki inataja kampuni zilizoko kwenye jengo hilo katika Kitalu Namba. 189/2 kwenye Barabara ya Nyerere kuwa ni Quality Group Company Limited, Gaming Management Limited, Q Consult Limited, Quality Logistics Company Limited na International Transit Investment Limited, ambazo ziko chini ya Manji.
Uamuzi wa kuyatimua makampuni ya Manji, Diwani wa Mbagala Kuu jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, unafuatia uamuzi wa shauri lililokuwa katika Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi ambao ulitolewa na Jaji Mgetta Novemba 24, 2016, ambapo pamoja na mambo mengine, iliamuliwa kampuni hizo ziondoke mara moja.
"Katika shauri husika, Mahakama iliamuru miongoni mwa mambo mengine, kuondoka mara moja kwenye eneo husika linalojulikana kama PSPF Plaza, zamani Quality Plaza, lililoko kwenye Kitalu Namba. 189/2 kwenye Barabara ya Nyerere. Unatakiwa uwe umeondoka kwa amani katika muda wa saa 24 kuanzia tarehe ya notisi hii. Zingatia kwamba, kama hutaondoka katika muda wa saa 24, Mfuko umemwagiza dalali Yono Auction Mart and Co. Ltd kukuhamisha kwa nguvu," imeeleza notisi hiyo ya Desemba 2, 2016 kwenda kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Quality Group of Companies.
Manji kwa sasa ni mshauri wa makampuni ya Quality Group baada ya kujiuzulu rasmi uenyekiti mnamo Julai 15, 2016.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK