Dk Shein na Maalim Seif Jino kwa Jino Zanzibar Leo,Watapanda Majkuwaani Kurushiana Maneno..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad watafunga mikutano ya kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge wa Jimbo la Dimani unaotazamiwa kufanyika jumapili.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Ofisi Makao Makuu ya CCM Kisiwandui jana Dk Shein atafunga mikutano ya kampeni za kumnadi mgombea wa CCM Juma Ali Juma ambaye anapewa nafasi kubwa ya kuibuka na ushindi.

Katibu wa Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar, Idara ya Itikadi na Uenezi Waride Bakari Jabu alisema kampeni hizo zitafikia tamani kwa Dk Shein kuhutubia mkutano wa mwisho wa kampeni.

“Kampeni zitafikia tamati kwa kupata baraka kubwa za Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar, Dk Shein,” alisema.

Juzi akizungumza katika mkutano wa kampeni Bweleo, mgombea wa CCM Juma alisema atahakikisha vikundi vya wajasiriamali wanawake vinapewa kipaumbele kwa kupatiwa mitaji ya kuendesha biashara zao.

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif anatazamiwa kufunga mkutano wa kampeni za uchaguzi mjini Fumba Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.

Chama cha CUF katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Dimani kimemsimamisha mgombea wake Abdulrazak Khatib. Jumla ya vyama vya siasa 12 vinashiriki katika uchaguzi huo huku chama cha CCM na CUF vikionesha kuwepo mchuno mkali.

Uchaguzi huo unafanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo Hafidh Ali Tahir (CCM) aliyefariki akiwa katika mkutano wa Bunge mjini Dodoma mwaka jana.

Mapema jana Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) ilisisitiza kwamba watu watakaopiga kura ni wale ambao wamesajiliwa katika daftari la kudumu la wapiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka. 2015.

Mkurugenzi wa ZEC Kassim Ali alisema ni matarajio yao kuwa wapiga kura na wananchi wa Jimbo la Dimani watashiriki katika uchaguzi mdogo kwa njia ya amani na kuheshimu demokrasia.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad