MaDj Wa Sauzi Waufagilia Muziki Wa Bongo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Siyabonga Sibeko ‘DJ Capital’ (kushoto) na Lutendo Kungoane ‘Dj Sliqe’ (kulia) wakizungumza na Waandishi wa Habari jana

WACHEZESHA disko ‘ma DJ’ maarufu Afrika Kusini Siyabonga Sibeko ‘DJ Capital’ na Lutendo Kungoane ‘Dj Sliqe’ wamesema kwamba muziki wa Tanzania uko juu kwa sasa.

Wakizungumza na Waandishi wa Habari jana katika hoteli ya New Africa, Dar es Salaam ma DJ hao wa Redio na Telesheni nchini Afrika Kusini walisema Tanzania imepiga hatua kubwa kimuziki.

“Kwa sasa huwezi kuzungumzia nchi zinazofanya vizuri kwa kiwango cha juu kimuziki Afrika bila kuitaja

Tanzanja,”alisema Dj Capital na kuongeza; “Afrika Kusini, Nigeria, Ghana, Tanzania na Kenya hizo ndizo nchi za Afrika zinazofanya vizuri katika muziki wa kisasa,”alisema.

Kwa upande wake DJ Sliqe’ alisema kwamba anavutiwa zaidi na wasanii wawili wa Tanzania kwa sasa, ambao ni Diamond Platnumz na Vanessa Mdee.

“Ni wasanii wengi wa Tanzania wanaofanya vizuri kwa sasa, lakini mimi upande wangu nawapenda zaidi hao wawili,”alisema.

Wawili hao, wote ni Ma DJ wa kituo cha Redio cha Touch Central cha Johannesburg, Afrika Kusini wakati DJ Capital pia anafanya kipindi cha Club 808 cha Televisheni ya ETV nchini humo.

Wawili ambao wamekuja nchini kwa ziara ya wiki moja kujifunza zaidi kuhusu muziki wa Tanzania, pia ni Ma DJ wa kumbi za disko nchin kwao.

“Tumekuja hapa kujigunza na kukutana na wasnaii kwa sababu sisi pia ni watayarishaji wa muziki,”alisema Capital.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad