Spika Ndugai Apokea Barua ya Kujiuzulu Ubunge ya Dk Abdallah Possi Aliyeteuliwa Kuwa Balozi..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Job Ndugai amepokea barua ya kujiuzulu Ubunge iliyowasilishwa kwake na Dokta Abdallah Saleh Possi aliyeteuliwa kuwa Balozi katika kituo atakachopangiwa hapo baadae.

Taarifa ya Spika Ndugai ya kuwaarifu wabunge wote na wananchi kwa ujumla iliyotolewa jana imesema barua hiyo ya kujiuzulu Ubunge wa Dokta Possi imezingatia masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 67(1) (g) ikisomwa pamoja na ibara ya 149 (1) (d), hivyo Spika wa Bunge amemwandikia rasmi Rais kuwa hivi sasa wabunge wa kuteuliwa na Rais waliopo Bungeni ni saba (7) na hivyo nafasi zilizowazi ni tatu (3) baada ya Dk Possi kujiuzulu.

Taarifa hiyo imetolewa na kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano ofisi ya Bunge.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad