BINTI wa Mugabe Kugombea Urais wa Zimbabwe..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Makamu wa Rais wa zamani wa Zimbabwe Joice Mujuru alikuwa swahiba mkubwa sana wa kisiasa wa Rais Robert Mugabe. Alikuwa mstari wa mbele kabisa kumtetea rais huyo na sera zake.

Mujuru mwenye umri wa miaka 61 alipandishwa wadhifa kutoka uwaziri hadi kuwa Makamu wa Rais mwaka 2004. Alikuwa mtetezi mkubwa wa Mugabe wakati uchumi wa nchi hiyo ulipokuwa unadidimia, na amekuwa akimuunga mkono na kumfanyia kampeni kali katika chaguzi tatu, chaguzi ambazo wapinzani nchini humo na watazamaji wa kimataifa walisema hazikuwa huru na haki.

Mwaka 2007 Mujuru aliwahi kuliambia gazeti la Telegraph la Uingereza kwamba kwa namna walivyokuwa karibu na Mugabe, alikuwa anajihisi kama ‘binti’ yake tu.

Lakini miaka mitatu baada ya kujiondoa kutoka chama tawala cha Mugabe (ZANU-PF) kutokana na madai kwamba alikuwa anapanga njama za kumuua Mugabe, mawasiliano kati yake na rais huyo yakatoweka kabisa.

Anasema tangu ajitoe kutoka chama hicho mwaka 2014, hajapigiwa simu na Mugabe, naye pia hajampigia simu – yaani hawajaongea kabisa.

Akiwa London wiki iliyopita akihamasisha Wazimbabwe walioko nje ya nchi kumtosa Mugabe, Mujuru aliliambia jarida la Newsweek kwamba hana mawasiliano na Mugabe kabisa na kwamba hajutii uamuzi wake wa kujiondoa ZANU-PF kwani aligundua kuwa Mugabe alikuwa anataka kumtumia tu kisiasa.

Mwaka jana 2016 alianzisha chama chake cha siasa – National People’s Party (NPP) – ingawa wapinzani wenzie wana shaka naye hasa kutokana na baadhi ya kauli zake za kusifia sera fulani za Mugabe.

Aidha katika mkutano mmoja mkubwa uliojumuisha vyama vya upinzani mjini Harare mwezi uliopita Mujuru hakuwapo jukwaani ingawa wafuasi wake wengi walikuwepo – kitu ambacho kilianzisha minon’gono.

Hata hivyo wachunguzi wa mambo wanasema uswahiba wa muda mrefu wa kisiasa uliokuwapo baina yake na Mugabe umemsaidia Mujuru kwa kumemjenga hadi kuwa mwanasiasa mashuhuri zaidi nchini Zimbabwe.

Lakini sasa hivi Mujuru anavyojitayarisha kugombea urais katika uchaguzi wa mwaka 2018, uchaguzi ambao wengi wanaona utatoa fursa ya mabadiliko makubwa ya kisiasa nchini humo, mwanamama huyo anakabiliwa na changamoto kubwa ya kuwaaminisha wananchi wake kwamba anaweza kuwaletea hali tofauti ya ile iliyopo chini ya ‘mlezi’ wake wa zamani – Mugabe.

Anasema katika uchaguzi ujao Wazimbabwe wataona uzoefu wake katika serikali ya Mugabe kama ni turufu ya kisiasa na siyo doa katika hadhi yake.

Anasema: “Wazimbabwe wamekuwa wananifahamu kwa muda mrefu, tangu nilipokuwa waziri mwenye umri mdogo, na wanafahamu vizuri jinsi nilivyokuwa natimiza wajibu wangu.”

Na sasa hivi Zimbabwe inakabiliwa na matatizo makubwa ya uchumi kwani haujatulia sawasawa baada ya mfumuko wa bei na kuanguka thamani ya sarafu yake (Dola ya Zimbabwe) mwaka 2008/2009. Wakati ule sarafu hiyo ilikuwa inaanguka thamani kwa asilimia bilioni 80 kila mwezi na mkate mmoja uligharimu Dola za Zimbabwe milioni 10.

Sasa hivi asilimia 63 ya Wazimbabwe wako chini ya mstari wa umasikini na robo ya wananchi wanakabiliwa na baa la njaa kutokana na ukame.

Wachumi wengi wanasema nyingi ya changamoto hizo zinatokana na sera mbovu za kiuchumi za kiongozi huyo. Kati ya 2000 na 2008, Pato la Taifa (GDP) la Zimbabwe’s lilianguka kwa asilimia 50 kwa mujibu wa takwimu za Benki ya Dunia.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad