KIMENUKAAA..Korea Kaskazini Watishia Kuizamisha Meli Vita ya Marekani Iliyoko Katika Rasi ya Korea..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


KOREA KASKAZINI jana imesema itaonesha uwezo wake mkubwa wa kijeshi kwa kuizamisha meli ya kubebea ndege za kivita ya Marekani iliyo njiani kuelekea rasi ya Korea.

Kauli hiyo imekuja baada ya meli mbili za japani kuungana na ya Marekani kwa mazoezi ya kivita magharibi mwa Bahari ya Pasifiki.

Rais wa Marekani, Donald Trump aliamuru meli hiyo USS Carl Vinson kuelekea katika rasi hiyo kufuatia majaribio ya makombora ya nyuklia ya Korea Kaskazini na tishio la shambulio dhidi ya Marekani na washirika wake wa Asia.

Marekani haijataja eneo hasa ambalo meli hiyo imefika, lakini Makamu wa Rais wa Marekani, Mike Pence alisema itawasili ndani ya siku chache bila kufafanua.

“Majeshi yetu ya mapinduzi yamejiandaa kuizamisha meli inayotumia nguvu za nyuklia ya Marekani kwa pigo moja,” Rodong Sinmun, gazeti la chama tawala cha Wafanyakazi nchini humo lilisema.

Gazeti hilo liliifananisha meli hiyo na ‘mnyama mchafu’ na kwamba pigo hilo litaonesha mfano halisi wa uwezo wa kijeshi wa Korea Kaskazini.

Katika kinachoonekana ongezeko la mgogoro baina ya pande hizo mbili, Korea Kaskazini imemkamata mtu mwenye asili ya Marekani na Korea na kufanya idadi ya Wamarekani wanaoshikiliwa mjini Pyongyang kufikia watatu.

Mtu huyo aliyejulikana kwa jina moja la Kim, amekuwa nchini humo kwa mwezi moja kwa shughuli za hisani, shirika la habari la Yonhap limesema.

Alikamatwa kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa Pyongyang wakati akijiandaa kuondoka humo.

Taifa hilo linatarajia kuadhimisha miaka 85 ya kuwekwa msingi wa jeshi lake la watu wa Korea kesho.

Huko nyuma maadhimisho muhimu kama hayo yamekuwa yakiendana na majaribio ya silaha.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad