AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Chanzo ya kwanza kabisa duniani dhidi ya ugonjwa wa Malaria inatarajiwa kutolewa katika nchi tatu za Ghana, Kenya na Malawi kuanzia mwaka 2018.
Chanjo hiyo ya RTS,S inafundisha mfumo wa kinga mwilini, kushambulia vimelea vya Malaria vinavyosambazwa na mbu, ambapo kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, chanjo hiyo ina fursa kubwa ya kuokoa makumi kwa maelfu ya maisha.
Lakini haijafahamika kama chanjo hiyo itaweza kutumika kwa nchi ambazo zina huduma duni za afya. Chanjo hiyo inatakiwa kutolewa mara nne yaani mara moja kila baada ya miezi mitatu na dozi ya nne miezi 18 baadaye.
Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika, Dk. Matshidiso Moeti, amesema chanjo hiyo inatarajiwa kutolewa kwa zaidi ya watoto 750,000 wenye umri wa kati ya miezi 5 hadi 17.
Licha ya mafanikio hayo makubwa, bado kuna visa vipya milioni 212 vya Malaria kila mwaka na vifo 429,000
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK