AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mwenyekiti wa Bodi ya Parole Tanzania, Augustine Mrema amesema kuwa uhalifu unaoendelea kujitokeza hapa nchini unafanywa kwa makusudi na watu wenye nia mbaya na Serikali ya awamu ya Tano.
Amesema kuwa uhalifu kama huo haukubaliki hivyo unatakiwa kupigwa vita na kila mtu mwenye mapenzi mema na nchi kwani haijawahi kutokea mauaji ya askari Polisi kama yaliyotokea hivi karibuni.
Ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na kituo kimoja cha redio Jijini Dar es salaam kuhusu hali ya nchi ilivyo kwa sasa, amesema kuwa kwa sasa ana mpango wa kuonana na Rais Dkt. Magufuli ili aweze kumuomba amruhusu kutoa wafungwa wenye sifa ya kupata msamaha ili waweze kusaidia kutoa taarifa za watu wanaofanya uhalifu huo.
“Kuwatoa wafungwa wenye sifa ya kupata msamaha itakua ni moja ya mkakati ambao utawezesha kukamatwa kwa wahalifu wanaondelea kufanya mauaji nchini, hawa wafungwa lazima watakuwa wanajua walipo wahalifu,” amesema Mrema.
Aidha, Mrema ameongeza kuwa atatumia mbinu zote na uzoefu alionao ili kuweza kupambana na uhalifu huo, kwani kulingana na uzoefu wake amegundua kuna kampeni za makusudi zinazofanywa kwa ajili ya kumchafua Rais Dkt. Magufuli.
Hata hivyo, katika hatua nyingine amemtaka Rais Dkt. Magufuli kuwashughulikia wale wote wanaoleta viashiria vya uvunjifu wa Amani hapa nchini.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK